Labels

Thursday, November 22, 2012

JE! MUNGU NA YESU NI MMOJA?


Makanisa ya Kikristo yanafunza ya kuwa Yesu Kristo si kama kuwa ni Mwana wa Mungu tu, bali hakika ni Mungu khasa.  Baba, Mwana na Roho Mtakatifu ni mmoja.  Watatu katika mmoja, na mmoja katika watatu.  Wote ni wa milele, wote ni sawa.  Yesu ni Mungu, na Mungu ni Yesu. Hiyo ni imani ya Kikristo, ambayo inaaminiwa na karibu Wakristo wote.  Hebu tuifunue Biblia tutazame inasema nini katika jambo hili?
Mt Paulo katika barua yake ya kwanza kuwapelekea Wakorintho aliandika:
Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.
1 Wakorintho 15.15
Juu ya kuwa Paulo anaambiwa ya kuwa akiamini kuwa Masihi (yaani Kristo) na Mwenyezi Mungu ni kitu kimoja hapa anasema: "Tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo." Ikiwa Mungu kamfufua Kristo, hawawezi kuwa wote wawili hao ni mtu  mmoja. Mmoja alikuwa ni mtenda, mfufuaji, na wa pili alikuwa ni mtendwa, mfufuliwa. Kama Kristo ni Mungu mwenye uwezo wa kufufua basi maelekeo ni kusema: "Kristo kajifufua", sio kafufuliwa. Mwenye kufufuliwa ni mfu asiyejiweza kitu.
Katika kitabu cha Matendo ya Mitume inasimuliwa kuwa Mt Stefano alisema aliyoyaona yaliyo mbinguni. Alisema:
Tazama!  naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
      Matendo 7.56
Mwana wa Adamu ndiye Yesu, na kwa jina hilo ndio mwenyewe akipenda kujiita, sio Mwana wa Mungu. Hapo basi huko mbinguni Stefano anasema anamwona Yesu kakaa mkono wa kulia wa Mungu. Mwenye kukaa mkono wa kulia wa fulani hawezi kuwa ndiye yule yule fulani. Hayo ni maelezo ya mbinguni.  Ni wazi basi kwa ushahidi wa Biblia kuwa Yesu hakuwa Mungu mbinguni kama alivyokuwa si Mungu duniani.
Yesu alipokimbilia kwenye Mlima wa Zaituni na huku akisakwa na Mayahudi alijitenga na wanafunzi wake.  Huko faraghani aliomba hivi:
Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.  Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.
  Luka 22.42-43
Hapa tunaona mambo matatu muhimu:
  1. Yesu anamwomba Mungu. Yesu anamwabudu Mungu. Wawili hao ni mbali mbali, na vyeo vyao ni mbali mbali. Yesu ni mtumwa mnyonge mwenye kuomba na kuabudu. Na Mungu ni Mwenyezi Mungu mwenye uwezo wote na mwenye kustahiki kuabudiwa pekee, hata na Yesu, mwenye kutakiwa msaada pekee, hata na Yesu.
  2. Mapenzi ya Mungu ni mbali na yale ya Yesu. Yesu hataki kuuliwa, ananyenyekea na kuomba kwa Bwana wake: "uniondolee kikombe hiki" cha mauti.  Yesu hana azma hata chembe ya kufa msalabani, kifo cha mhalifu, kifo cha laana kama maadui zake  Mayahudi walivyoazimia kumpatilisha nacho. Lakini anakiri kuwa ni mapenzi ya Mungu sio yake yeye yatendeke. Yeye hana hila wala nguvu za kuzuia kudra ya Mwenyezi Mungu.
  3. Yesu, Mwana wa Adamu, anakata tamaa. Imani inampunguka. Kavunjika moyo. Ikabidi "Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu."
Jee, yaelekea kuwa Yesu ndiye Mungu? Yaelekea kuwa yeye na Mungu kuwa ni sawa? Kama upo wasiwasi wo wote wa kujibu hayo, mwenyewe Yesu anajibu kama anavyo hadithiwa na Yohana kuwa kasema:
Baba ni mkuu kuliko mimi.
Yohana 14.28
Na mwishoni naye yupo mslabani:
Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani?  yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?
Mathayo 27.46
Yafaa hapa tujiulize: Yesu akimlilia Mungu gani hapo msalabani ikiwa naye mwenyewe ni Mungu? Au nini alikusudia aliposema: "Mungu wangu naye ni Mungu wenu"?  Maneno hayo kama yanaonyesha cho chote basi yanaonyesha unyenyekevu wa Yesu mbele ya Mungu wake.  La kustaajabisha ni kule kukata tamaa kwake na kuvunjika moyo.  Huwaje mtu wa imani, licha ya nabii na mwana pekee wa Mungu, akate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu.  Ama kuwa Mungu akate tamaa na Mungu, na kumyayatikia: "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha", ni jambo ambalo halimkiniki kuwa.
Kwa uthibitisho ulio wazi Biblia inatwambia kuwa Yesu si Mungu, wala Mungu si Yesu. 

Tuesday, November 13, 2012

FAHAMU NINI MAANA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA BIBLIA

 Mt. Meshack Ezekia Kitova    phone;0757672626

 Nini maana ya kusifu na kuabudu


KUSIFU NA KUABUDU ni maneno tofauti na yana maana tofauti
1. kusifu

MAANA --- nikuelezea wasifu au wajihi za kitu au mtu. Sasa tunaposema tunamsifu Mungu inamaanisha ni KWA KUMUINUA JUU, KUSHUKURU KUMPAZIA SAUTI,KUFANYIA SWANGWE, KUJISHUSHA CHINI YAKE KWA UNYEYEKEVU,nk Zaburi 100:4

Neno hili kusifu kwa kiebrania lilikuwa na maana ya;
Tehila, yaani kutamka neno kwa kuongeza vionjo na mbwembwe zaidi. Mfano neno haleluya unalitamka (Ha, ha leluya huuu eee) Tehila ni kuwa kama kichaa unaposifu au kuabudu kwa utukufu wa Bwana. (Nilidhani labda hapa ndipo waswahili walipopata neno taahila).

Yadaa yaani kujiachia kwa Mungu (you just surrender yourself to the Lord).
Barak yaani kusaluti mbele za Bwana. Ni kuonyesha kwamba ni yeye peke yake anayestahili heshima na utukufu. Huwezi kumpigia saluti mtu usiyemwona, hivyo ni kwa njia ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli ndipo tunapomwona kama alivyo na utukufu wake

2. Kuabudu
Neno la Kiebrania shachah lina maana ya kuabudu, kusujudia, kuinama kwa kuonesha unyenyekevu, kuonesha heshima kubwa au kuanguka kifudifudi. Neno la Agano la Kale proskuneo halikadhalika lina maana ya kubusu mkono, au kupiga magoti na kugusa ardhi kwa paji la uso kwa unyenyekevu mkuu. Maneno mengine mawili ya kuabudu yana maana ya kutumika, kufanya ibada Takatifu na kumtolea Mungu Sadaka.

Waache Watu Wangu Waondoke, Ili Wapate Kunitumikia, Dai hili Mungu alilolirudia mara kwa mara lilipelekea Farao kuwaruhusu watu wa Mungu kutoka Misri. Tangu wakati huo, Mungu, Mungu mwenye wivu, amekuwa akipambana na watu wake akiwazuilia kuabudu miungu mingine na sanamu, na badala yake wamwabudu Mungu aliye hai na wa kweli. Kutoka 7:16
Ibada ni kumtukuza Mungu na kumfurahia daima. Mungu anawatafuta watu wa kumwabudu, na kufanya ibada ndiyo wito wetu wa kwanza (Yn4:23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta. Msitari wa 24 unasema Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.). Ibada ya kweli ni pale tunapomruhusu Roho Mtakatifu atuongoze kutoka katika roho zetu au mioyo yetu kuabudu katika roho na katika kweli na sio tumaini letu ktk miiliau akili zetu Flp 3:3.

Ibada ni tendo la thamani kubwa, ni la kipekee na linamhusu Mungu (utatu mtakatifu) ambao peke yao wanastahili. Lucifer, aliyekuwa mhusika mkuu wa ibada huko mbinguni, alitaka ibada hiyo iwe kwa ajili yake, maana yake aabudiwe yeye badala ya Mungu; na hilo ndilo lililopelekea kuanguka kwake (Isaya 14 na Ezekieli 28). Hata wakati fulani alitaka Yesu amsujudie ili eti ampe falme zote za dunia lakini Bwana alikataa Mt4:8-10.

Kwa hiyo kuabudu ni ibada na tunaposema ibada sio zile taratibu za kibinadamu tulizojipangia katika ibada zetu za siku za leo, ibada za leo tumeweka mambo mengi sana na yanatumia muda mwingi sana kuliko ile maana hasa ambayo mungu aliikusudia katika agano la kale utana ibada zilikuwa zinafaywa kwa mambo makuu 2 neno la Mungu, na Kuabudu.

Kuabudu ni sehemu ya maisha wanadamu tumeumbiwa kuabudu, watuwezi kuishi bila kuabudu hapa haijalishi unaabudu nini!!! Unaweza kuwa unaabudu Mungu wa kweli au miungu kama ambavyo ukisoma bilia utaona kuna miungu mingi inatajwa mfano Baali, Dagon ink na hata leo iko miungu mingi ambayo wanadamu wanaiabudu lakini wa kuabudiwa ni mmoja tu. Na katika biblia tunaona kuaudu kwa mara ya kwanza kulikofanywa na Ibrahimu kutoka katika kitabu cha mwanzo 12: 8 Psalms 34:1 inaonyesha tunatakiwa kumwabudu Mungu kila wakati.

Kwanini tuabudu
kuabudu ni agizo kutoka kwa Mungu kutoka 20 2-4 . Psalm 96:9, Psalm 29:2 Tunapomwabudu mungu naye Mungu hufurahiwa na sisi Zephaniah 3:17 Rom 12:1-2

Your Worship = Your View of God
jinsi unavyoabudu ndiyo mwonekano wa mungu ulivyo ndani yako, haijarishi unaabudu wapi uwe peke yako au mko wengi kama unaabudu kwa kutokumaanisha au kumaanisha itajulikana tu na hivyo ndivyo mtu anaweza kujua ni jinsi gani mtazamo wako kwa Mungu wako.

KUNA NGUVU KATIKA KUSIFU NA KUABUDU
Yoshua 6:20 Matendo 16:23-26 zinaonyesha ambavyo kwa kutumia kusifu tu Mungu alishuka na kufanya lile lililokuwa hitaji lao.

Kusifu kunamfukuza adui
Psalms 50:23. 2 Nyak 20:22. Ukiwa unasifu na kuabudu humfukuza adui mbali kutokana na ukiwa kwenye ibada Mungu hushuka maana yeye anasema anakaa katikati ya sifa hivyo palipo na Mungu shetani hawezi kuwepo lazima akae mbali.akimbie mbali kabisa maana kunakuwepo na uwepo wa bwana wa Majeshi.

Je, ni wakati gani tuabudu?
Ni niyakati zote zinafaa kumwabudu Mungu. Kwa nyakati zilizotengwa Zaburi ya 100 inatuelekeza namna ya kuanza, lakini zaidi ya yote tunapaswa kuishi maisha ya ibada bila kukoma. Kwa kila tunapopumua, kwa kila wazo, kwa neno na tendo, tunapaswa kumwabudu Mungu wetu mzuri tunayemtumikia milele na milele Zab 145:1,2

mwa 12:6- Siku zilipita na watu wakafanyia ibada kwenye Hekalu na kwenye masinagogi; lakini siku hizi miili yetu ni hekalu la Mungu 1Kor 6:19 tu hekalu la Mungu sisi ibada zinatakiwa zifanyike kila wakati na si mara moja kwa wiki kama wengine wanavyo dhani.

Je, Tunafanyaje Ibada?
Biblia inatufahamisha jinsi watu walivyotumia mioyo yao, mawazo yao, mikono yao, viganja vyao, miguu yao, na midomo yao katika uimbaji. Walipaza sauti zao kwa furaha na kusujudu, kucheza, kusifu, kubariki na kushukuru.

Maneno kama halal na haleluya kutoka katika Zaburi yana maana ya kusifu, kumwinua na kumwadhimisha Bwana. Neno Yadah lina maana ya kunyoosha mikono hewani, na neno barak lina maana ya kupiga magoti katika ibada ya kumbariki Mungu. Kuitoa miili yetu katika kumhudumia Mungu na mwanadamu ni ibada pia (Rum 12:1). Watu pia humwabudu Mungu katika sanaa zao, katika uandishi wao, katika michezo ya kuigiza, katika muziki, katika usanifu wa majengo, na hata katika utoaji wa fedha zao kwa ajili ya Injili.

Kusifu na kuabudu sio kuimba tu
Watu wengi wanajua kuwa kusifu na kuabudu ni kuimba tu hapana kuna njia nyingi za kusifu au kuabudu, unaweza kutumia sanaa nyingine kumwabudu mungu au watu wengine wakamwabudu Mungu mf maigizo, ngonjera, shaili, uchoraji, upambaji au unakshi wa vitu, kujenga .nk

Ibada Kanisani
KatIka kanisa makusanyiko yetu yanapaswa kujawa na zaburi, nyimbo, na tenzi za rohoni ambazo zinaweza kuongozwa na Roho katika lugha mpya anazotupatia Yeye. Kwahiyo mikutano mingi ya kisasa haina tofauti sana na burudani za kikristo kama kwenye kumbi za starehe. Watu huwa wanaangalia tu, lakini je, wanaabudu? Uwepo wa Mungu na Roho wake katika ibada zetu utawafanya watu wasioamini kuanguka chini na kuabudu (Kol 3:16) (1Kor 14:15,16,25,26) (Efe 5:19) (Mdo 2:4).

Ibada Ya Kweli Ina Gharama
Biblia inazungumzia habari za sadaka za kusifu. Daudi alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote, na akakataa kumtolea Mungu kafara ambayo isingemgharimu cho chote (2Sam 6:14; 24:24). Wale mamajusi wa Mashariki walitoa zawadi za gharama kubwa walipokuja kumwabudu Yesu (Mt 2:9-12), na mwanamke mmoja alimpaka Yesu kwa mafuta ya gharama kubwa, akamwosha miguu yake kwa machozi yake, na kuifuta kwa nywele zake (Lk 7:36-50). Hivyo ibada yoyote inaambatana na kutoa tena vitu vyetu vya thamani.

Tunapaswa kumsifu Mungu kwa jinsi alivyo na kwa matendo yake; lakini Mungu mwenyewe anawatafuta na anawataka wafanya ibada, na si mradi ibada tu. Kusifu kwaweza kufanywa hadharani, lakini ibada mara zote ni jambo la ndani ya moyo. Kusifu mara zote kunaweza kuonekana au kusikika, lakini kuabudu yaweza kuwa ya kimyakimya na iliyofichika. Kusifu kunaonekana, kuna kutumia nguvu, kuna misisimko na furaha; lakini ibada mara zote ni heshima na hofu katika uwepo wa Mungu.
Biblia pekee inatuonesha jinsi Mungu anavyo hitaji na kutamani kuabudiwa na yeye pekee yake ndiyo anayestahili kuabudiwa.

Kusifu na kuabudu kwa siku za leo
Katika siku za leo kuna ufinyu wa mafundisho katika kusifu na kuabudu na ndiyo maana ya kuanda somo hili ili tupanuane mawazo. Watu wengi wa leo wanadhani kusifu ni kuimba kwa nyimbo zenye midundo ya harakaharaka(zouk&sebene) na ukipunguza spidi ndo kuabudu. Hasha tunaposema kusifu inatokana na maneno yaliyopon kwenye wimbo husika kweli ni ya kusifu, kama ni maneno ya kusifu tunasema ni wimbo wa sifa haijarishi speed inayotumika na hali kadhalika nyimbo za kuabudu. Watu katika kipengele hiki huwa wanachakanya nyimbo utakuta wakati wa kusifu anaimba wimbo wa kutia moyo au wa maombi, kinachotakiwa ni kujua kuwa kila jambo lina wakati wake ziiko nyimbo za mazishi, kufariji, kutia moyo, za maombi, za kusifu , na za kuabudu nk sasa usichanganye kwenye kusifu wewe unaimba parapanda italia au tuonane paradiso, hizo sio za sifa sasa najua wewe utafanya zoezi la nyimbo unazozijua ili kufahamu zina ujumbe gani na ziko katika kundi lipi kati ya hayo niliyokufundisha hapo juu.

Baadhi ya maandiko yanayo onyesha aina za kusifu na kuabudu kwa:

1. Kusimama (Zab 135:1-2, 134:1)

2. Kuinua mikono (Zab 134:2, 28:2)

3. Kuinama au kupiga magoti (Zab 95:6)

4. Kupiga makofi (Zab 7:1)

5. Kucheza (Zab 149:3, 150:4, 2Sam 6:14)

6. Kicheko (Zab 126:2, Ayu 8:20-21)

7. Kufurahi (Kumb 12:11-12, Law 23:40)

8. Kutembea (2Nya 20:21-22)

9. Shangwe (Zab 95:1)

10. Kupiga kelele (Zab 66:1, Law 9:23-24)

11. Kupiga vigelegele (Zab 33:1, 32:11)

12. Ukimya (Mhu 3:7)

13. Kupaza sauti (Isaya 12: 6, Zab 42:4)

14. Kulia/ kutoa machozi katika roho mtakatifu

Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa

Mpango Wa Mungu Kwa Ulimwengu


Katika Biblia Yako SomaIsaya 66; Zaburi 67.
Mstari wa Kukariri
 ‘
…wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia,”Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa; usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike,kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu,naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.” (Isa 41:9,10).
Baadaye Zungumzieni Jambo HiliMwambie mwenzako Msalaba unaweza kumaanisha nini kwako kwa kile ambacho Mungu anaweza kukitaka kwako; pengine atataka uende mahali fulani, au atakuamuru kufanya jambo fulani,  au atakuamuru kutoa kitu fulani, au atakuamuru kuacha jambo fulani.
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana TenaKwa kuzingatia kwamba muda unakwenda mbio na siku ya mwisho inakaribia, hebu fanya maombi kwa upya ukimkabidhi Yesu wenye dhambi wawili kutoka kwenye familia yako au miongoni mwa rafiki zako.
Kazi ya Kuandika Ya StashahadaJe, unauhisi mkono wa Mungu ukiwa juu ya maisha yako ukikuchagua kumtumikia Yesu? Andika ukurasa mmoja wenye maelezo ya kile unachofikiri  Mungu anakuitia. Je, unafikiri anakuita uwe nani au ufanye nini?
Tafakari Mistari IfuatayoIsa 43:4-7
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea Falme za Kiarabu.
Wapo Waislam 2,200,000 katika majimbo 7; Kuna umaskini kwenye utajiri mkubwa Huduma ya Kikristo imekatazwa; Hakuna Kanisa nchini humo

Hakikisha umewafundisha wengine somo hili.
Kila mara omba na kujiandaa ukiongezea mistari mingine ya Biblia
na mifano yako mwenyewe ili kufanya somo lieleweke vizuri zaidi.

Kwa kawaida tunapenda kuhusisha Agizo Kuu na maneno ya mwisho aliyoyasema Yesu katika Injili zote, na hasa Mt 28:16-20, na katika Matendo.
Katika kitabu cha Mwanzo, Baba Mungu aliyesalitiwa na kuhuzunishwa, anatembea bustanini wakati wa jua kupunga akiwatafuta rafiki zake, mwanamume na mwanamke; ambao muda mfupi tu uliopita wamepoteza imani yao, kwa kuamua kumtii Shetani na kusababisha madhara makubwa kwa ulimwengu. Maneno ya Baba yanaelezea upendo wake, ‘Adamu uko wapi?’ Na kwa swali hilo haielekei kama Mungu alikuwa anataka kujua alikokuwa amejificha Adamu! Biblia inatuonesha kwamba Mungu alianza kuweka mambo sawa kwa kutoa ahadi (Mwa 3:9).
Katika kitabu cha Mwanzo pia kuna habari za Yusufu, mtu aliyetumwa na Mungu kuokoa taifa (Mwa 37-50).
 
Katika kitabu cha Kutoka, Mungu anaonesha uwezo wake wa kuokoa taifa kutoka utumwani. Anataka kuwabariki kwa kuwafanya taifa la kimishenari kwa kulipeleka Neno lake na uzima wake kwa ulimwengu wote (Kut 3:7-19:6).
 
Katika Zaburi, Mungu ameuonesha upendo wake mara kwa mara (Zaburi 67, Zaburi 2, Zab 72:17).
 
Manabii na manabii wadogo kama Yona walijazwa na uwezo wa kimbingu, japo kwa vipindi vidogovidogo, wa kuupenda ulimwengu (Isa 6:1-8; Isa 54:1-5; Hab 2:14)..
Mpango wa Mungu kwa ulimwengu wote unadhihirishwa na Nabii Isaya anaposema kwamba kuna mambo manne anayokusudia Mungu kuyafanya; vilevile yapo mambo mawili ambayo Mungu anataka sisi tuyafanye (Isa 66:18-21).
1. Mungu anasema, ‘Ninakaribia Kuja’
Katika Isa 66:18, huu ni ufunuo wa kinabii kuhusu Kuja Mara Ya Pili kwa Kristo.  Wakati huo atawakusanya mataifa yote pamoja kutokana na vitendo vyao na hisia zao. Hakuyafanya hayo alipokuja mara ya kwanza. Tutalijadili hilo baadaye na kuona ishara duniani na katika Ufalme zinazoashiria kurudi kwa Yesu.
Maana yake ni kwamba ipo siku ya mwisho. Hizi ni habari njema kwa kila mwamini, lakini pia ina maana kwamba kuna siku ya mwisho kwa kila mmoja wetu kuwaleta kwa Yesu jamaa zetu, rafiki zetu, na mataifa.
2. Nitafanya Ishara Miongoni Mwao
Ishara katika Isa 66:19 ni Msalaba, na huu unajulikana ulimwengu mzima. Kwa asiyeamini, Msalaba ni tamko la dhahiri la upendo mkuu wa Mungu kwa ulimwengu wote (Yn 3:16) Lakini kwa kila aaminiye, Msalaba una maana kubwa zaidi. Kalvari ilianzia Gethsemane na Yesu katika ubinadamu wake Msalaba ulimaanisha mapambano ya:
Kwenda asikotaka kwenda,
Kufanya asichotaka kukifanya,
Kutoa asichotaka kukitoa.
(Mt 26:39) (Lk 9:23)
Hapakuwa na njia nyingine. Na kwa furaha iliyokuwa mbele yake, furaha ya kukuona wewe ukiwa salama mbinguni, Yesu aliuvumilia Msalaba. Sisi nasi yatupasa kuvumilia kwa ajili ya wengine (Ebr 12:2).
3. Nitawapeleka Katika Mataifa Baadhi ya Wale Waliopona
Mbali sana; Hispania, Libya, Asia, Ugriki,na baadhi ya visiwa (Isa 66:19). Leo hii watu wa makanisa ya mataifa yaliyoendelea wanafanana sana na watu wa ulimwengu na ambao hawajafikiwa na Injili. Kwa ajili ya hao Yesu ataita watu na kuwatuma mbali sana kama wamishenari.
Je, unapaswa kupona nini?
Unapona mateso ya Msalaba na hitaji lake la kifo na kufanya mapenzi ya Mungu kwa gharama zote (Lk 9:23).
 
Unaponaje?
Ni ajabu, unapona tu na kuokoa maisha yako kwa kukubali kupoteza maisha yako kwa ajili ya Yesu na mapenzi ya Mungu (Lk 9:24).
Sasa tutaangalia na kuona yale mambo mawili ambayo tunapaswa kuyafanya ikiwa ni mwitikio wetu kwa wito wa Mungu wa kutumwa. Mambo yenyewe si magumu sana.
4. Watautangaza Utukufu Wangu
Je, utukufu wa Mungu ni nini? Ni Mungu aishiye Mwenyewe. Tunatangaza uwepo wake, upendo wake, nguvu zake, uweza wake, huruma zake na neema yake. Tunamtangaza Mwanaye, maisha yake, kifo chake, kufufuka kwake, na kwamba yu hai leo na anaweza kuokoa, kusamehe, kuponya, kuweka huru, na kuwajaza watu na Roho wake. Na ndipo utukufu wake unakuwa dhahiri kwa maisha yaliyobadilishwa (Isa 66:19; Mdo 1:8).
5.Watawaleta Ndugu Zako Wote
Mara zote Injili itafanya kile kilichoahidiwa kwenye Injili, na mwitikio wa watu ni kumfuata Yesu (Isa 66:20; Yn 12:32). Tutawaleta hadi mlima wake mtakatifu-hili likimaanisha ufuasi miguuni pa Yesu, (k.m. Mt 5:1).
Je, waamini wapya watatoka wapi?
Watakuja wamepanda farasi - ikiwa na maana ya mataifa ambayo hayajafikiwa ya Asia ya Kati. Tangu mwanzo farasi wengi walitokea eneo hilo.

Watakuja wamepanda magari
- ikiwa na maana ya watu waliorudi nyuma kutoka mataifa ya Magharibi.

Watakuja wamepanda vihongo
– ikimaanisha watu kutoka mataifa yanayoendelea.

Watakuja wamepanda ngamia
– ikiwa na maana ya watu kutoka mataifa ya Kiarabu kwenye Uislamu.

6. Nitachagua Baadhi Kuwa Makuhani
Hatua ya mwisho ya ufunuo wa Nabii Isaya ipo katika mstari wa 21 (Isa 66:21).  Ni unabii ulio sahihi kabisa kuhusu mambo ambayo Mungu anayafanya sasa katika ulimwengu mzima. Anawaita wanaume na wanawake walioamua kumfuata Bwana, kutoka watu wa mataifa yote na tamaduni  zote, kuacha yote na kumfuata Yesu. Tunaweza kumwona mwamini mchanga akipambana ili kuwa huru na dhambi, lakini Yesu anaona uwezekano wa mwamini huyu kuwa mtu wa Mungu, na anamchagua kuhudumu (Mk 1:17).
Mordecai Ham ni Mwinjilisti Mmarekani ambaye hakujulikana sana; na katika kuhubiri kwake katika mji mmoja zamani sana, hakujua kwamba kijana mmoja aliyetoa maisha yake kwa Yesu jioni ile baadaye angekuwa mhubiri mkubwa akiwahubiria mamilioni ya watu kote ulimwenguni katika muda mrefu wa huduma yake. Je, wamfahamu kijana huyo? Alikuwa ni Billy Graham ambaye jioni ile Mungu alimchagua kwa makusudi yake matakatifu.

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu
Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili Ya Yesu Kristo

Burkina Faso
Jina la Watu
Lugha Yao
Idadi Yao
Djan (Dian, Dyan)
Dian
14,100
Seemogo
Sambla (Seeku)
17,000
Senabi (Niangolo)
Senoufo, Senar (Nyangola)
50,000
Syem (Karaboro, Western, Syer)
Karaboro, Western
19,500  

Wednesday, November 7, 2012

Prayer for Salvation


1 God Loves You!

The Bible says, "God so loved the world that He gave His one and only Son, that whoever believes in Him shall not perish, but have eternal life"
The problem is that . . .

2 All of us have done, said or thought things that are wrong. This is called sin, and our sins have separated us from God.

The Bible says “All have sinned and fall short of the glory of God.” God is perfect and holy, and our sins separate us from God forever. The Bible says “The wages of sin is death.”
The good news is that, about 2,000 years ago,

3 God sent His only Son Jesus Christ to die for our sins.

Jesus is the Son of God. He lived a sinless life and then died on the cross to pay the penalty for our sins. “God demonstrates His own love for us in that while we were yet sinners Christ died for us.”
Jesus rose from the dead and now He lives in heaven with God His Father. He offers us the gift of eternal life -- of living forever with Him in heaven if we accept Him as our Lord and Savior. Jesus said "I am the way, the truth, and the life. No one comes to the Father except by Me."
God reaches out in love to you and wants you to be His child. "As many as received Him, to them He gave the right to become children of God, even to those who believe on His name." You can choose to ask Jesus Christ to forgive your sins and come in to your life as your Lord and Savior.

4 If you want to accept Christ as your Savior and turn from your sins, you can ask Him to be your Savior and Lord by praying a prayer like this:

"Lord Jesus, I believe you are the Son of God. Thank you for dying on the cross for my sins.  Please forgive my sins and give me the gift of eternal life.  I ask you in to my life and heart to be my Lord and Savior. I want to serve you always."

Did you pray this prayer?

YES NO

Je inamaanisha nini kuwa Mungu ni upendo? Je inamaanisha nini kuwa Mungu ni upendo?

Swali: "Je inamaanisha nini kuwa Mungu ni upendo?"

Jibu:
Hebu tuweze kuangalia vile Bibilia inaelezea upendo, na kisha baadaye tutaangalia namna chache vile Mungu ni sehemu kuu ya upendo. “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabiri; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. Upendo haupungui neno wakati wo wote” (1Wakorintho 13:4-8a).Hii ndilo elezo la juu sana la Mungu kuhusu upendo, na kwa sababu Mungu ni upendo (1Yohana 4:8) hivi ndivyo ilivyo.

Upendo (Mungu) hajilazimishi/haujilazimishi kwa mtu yeyote. Wale wanaokuja kwake wanafanya hivyo kwa kuitikia upendo wake. Upendo (Mungu) huonyesha upole kwa watu wote. Upendo (Yesu) alizunguka kote akifanya mazuri kwa watu wote bila upendeleo. Upendo (Yesu) hakutamani kitu cha wengine walikuwa nacho, aliishi maisha ya unyenyekevu bila kunung’unika. Upendo (Yesu) hakujivunia vile alivyo kuwa kimimwili, ingawa aliweza kumshinda nguvu kila mtu aliyekutana naye. Upendo (Mungu) haulazimishi unyenyekevu. Mungu hakulazimisha Mwnawe kunyenyekea, lakini kwa mubadala Yesu kwa pendo lake alimtii Babaye wa mbunguni. “Lakini ulimwengu ujue ya kuwa nampenda Baba; na kama vile Baba alivyoniamuru; ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, twendeni zetu” (Yohana Mtakatifu 14:31). Upendo (Yesu) alitwaza/na huwaza yaliyo mazuri kwa matakwa ya wengine.

Tibitisho kuu la upendo wa Mungu limeelezwa kwetu sisi katika Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” Warumi 5:8 yakiri ujumbe sawa na wa Yohana: “Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.” Tunaweza kuona kutoka aya hizi kuwa nia kuu ya Mungu ni tuwe pamoja naye katika mji wake wa milele, mbinguni. Ameifanya njia rahisi kwa kulipa gharama ya dhambi zetu. Anatupenda kwa sababu alichagua kwa kutekeleza kifungu cha nia yake. Upendo husemehe. “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” (1Yohana 1:9).

Je inamaanisha nini Mungu ni upendo? Upendo ni sehemu kuu ya Mungu. Upendo ni sehemu kuu ya tabia ya Mungu, na utu wake. Upendo wa Mungu kwa vyovyote vile haugongani/hitilafiana na utukufu wake, utakatifu na haki yake hata gadhabu yake. Sehemu zote za Mungu kwa pamoja zimekamilika. Chochote Mungu anatenda hupendeza, haki kwa sababu kila afanyacho hukifanya kwa haki na usawa. Mungu ni mfano mtakatifu wa upendo wa kweli. Cha kushangaza, Mungu amewapa uwezo wa kupenda vile anavyo penda, kupitia nguvu za Roho Mtakatifu wale wote watakaomkubali Mwanawe kama mwokozi wa maisha yao. (Yohana 1:12; 1Yohana 3:1, 23-24).