Labels

Sunday, May 18, 2014

UWEZA WA NENO LA MUNGU/power of word of God

po umuhimu wa kujua neno la Mungu katika maisha ya Mkristo halisi.
 
Biblia  inatuambia Yesu Kristo ndiye Neno la Mungu. Kwa maneno mengine Yesu ndiye Neno ambalo Mkristo anapaswa kuwa nalo (Yohana 1:1).

Kwa kusema hivyo kuna  umuhimu wa kumjua Yesu na kumshika, kwa maana yeye ndiye Neno la Mungu. Katika Biblia mtume Petro anasema mbele za Yesu kwamba, twende kwa nani na wewe ndio mwenye maneno ya uzima? Petro alijua upo umuhimu wa kumjua Yesu kama Neno maana ndani ya Neno kuna uzima
Biblia inasema neno la Kristo likae kwa wingi ndani yetu (Wakolosai 3:16).
Kwa nini basi neno la Kristo likae kwa wingi ndani yetu? Ni kwa sababu lina mambo yafuatayo ambayo ni muhimu katika maisha yetu ya Ukristo. Mambo hayo ni…
A) Neno la Mungu li Hai
B) Neno la Mungu lina nguvu (Mwanzo 1:6).
C) Neno la Mungu lina ukali kuliko upanga
D) Neno la Mungu linachoma hata kuzigawanya nafsi, roho viungo na mafuta yaliyomo ndani yake
E) Neno la Mungu li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo


KWA NINI NENO LA MUNGU LI HAI?
Neno la Mungu li hai kwa sababu  Mungu mwenyewe analithibitisha kwamba li hai maana 
a) Linafanya mabadiliko (Isaya 55:10-11).
b) Linatupa kushinda dhambi (Zaburi 119:11).
c) Neno la Mungu  li hai kwa sababu linatupa mafanikio katik mwili. Petro anasema ”kwa neno lako tunatupa nyavu zetu.“  Hapa tunaona kuwa Neno la Mungu  pekee yake ndilo linaloweza kuleta majibu katika maisha yetu (Luka 5:3-6).


Uhai wa Neno la Mungu kwa mtu ndio unaoleta kushinda dhambi. Nao wakamshinda kwa neno la ushuhuda wao (Ufunuo 12:11).

Daudi aligundua au kwa maneno mengine alifahamu umuhimu wa neno la Mungu katika maisha, kama vile mtume Paulo anavyosema na Wakolosai kwa habari ya neno la Kristo kwamba likae kwa wingi ndani ya mioyo yetu

Neno la Mungu lina nguvu na ndio maana  tunamshinda  shetani kwa neno la Mungu.
Yesu kama kielelezo yeye mwenyewe ni neno ndani ya neno anamshinda shetani (Luka 4:1-12). 


Katika mistari hiyo tunaona Yesu anamwambia  shetani  ”imeandikwa“   Shetani nae anageuza usemi nae anamwambia Yesu ”imeandikwa kwamba atakuagizia malaika usije ukajikwaa mguu wako.“ Kwa kuwaYesu neno la Mungu limo ndani yake hamwambii tena shetani imeandikwa ila anamwambia imenenwa. Kwa maneno mengine tukiwa na neno la Yesu ndani yetu hatuwezi kuyumbishwa. Kwanini? Kwa sababu tumeshaona jinsi ambavyo shetani  anajaribu kutumia neno la Mungu   kwa kusema ”imeandikwa.“  Na ni kweli imeandikwa ananukuu kutoka kitabu cha Zaburi 91 :1-12. Hata kama shetani ananukuu maandiko haina sababu  yamimi kushindwa na shetani  maana Yesu tayari alikwisha mshinda. Yesu kumshinda shetani ina nipelekea mimi kusoma neno la Mungu kwa bidiisana. Kwa mfano, ni kweli kabisa imeandikwa mtakula vitu vya kufisha havitawadhuru lakini je, ninywe sumu sitakufa kwa sababu imeandikwa? Hapana, ukinywa hakika utakufa. Shetani hutumia mandiko kuwafunga wasiojua neno la KristoYesu. 

Katika Biblia tunasoma pia kwamba ”imeandikwa“ Wanandoa MKE na MUME wasinyimane. Kwa kutojua neno vijana wa kiume na wa kike wamedanganywa. Si hao tu hata walioko kwenye ndoa wametegwa kwa andiko hilo. Neno linasema katika Mithali 6:32 ”Aziniye na mwanamke hana akili kabisa“ na Mwanamke vivyo hivyo akizini na mwanaume hana akili kabisa. Watu wamepata hasara ya mambo mengi kwa kutojua neno la Mungu. Ili tuweze kumshinda shetani  ni lazima  neno la Yesu liwe ndani  yetu ndiposa tutamshinda shetani. Ayubu kwa neno la Mungu alishinda. (Ayubu 19:25-27, Waefeso 6:17).

Nataka nikwambie neno la Mungu ni msaada katika maisha yetu maana hutupa  majibu ya maisha yetu. Katika Luka 5:3-6 tunasoma jinsi Petro na wenzake walivyopata samaki wengi kwa kutii neno la Kristo. Kumbuka pia juu ya yule akida, alimwambia Yesu ”...sema neno tu na mtumwa wangu atapona“ (Luka 7:2-10). Yesu akisema neno lazima mabadiliko yatokee. 

Neno la Mungu lina ukali kuliko upanga. Kwa nini neno la Mungu  lina ukali kuliko upanga? Upanga unaweza kukukata na usipone. Lakini neno linakata na kuponya. Kwa neno hili wafalme wanatubu. Yona alitumia neno la Mungu likawa kali watu wakatubu. (Yona 3:1-10; Matendo ya Mitume 8:18-24).

Neno la Mungu linachoma hata kuzigawa nafsi na roho na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake (Matendo 7:51-54, Yohana 4:16 -18, 27-29). Mwanamke akaambiwa mambo yake; Neno likachambua kila tabia..

Neno la Mungu li jepesi kutambua mawazo na makusudi ya moyo.
Yesu kama Neno la Mungu anajua mambo ambayo watu wanawaza ndani ya mioyo yao (Luka 5:17-24, 6:6-8 ; Mathayo 16:1-4)Yapo makusudi ya moyo ambayo ni ya siri sana kwa mwanadamu lakini nataka nikuambie neno la  Mungu ni jepesi kutambua makusudi ya moyo. 


Mtume Petro aliyependa kujua neno la Mungu, naye pia Mungu alimjalia neema ya kuyajua makusudi ya moyo wa mwanadamu (Matendo 5:1-11). Elisha aliyajua makusudi ya moyo wa mfalme ya kuwatenda Israeli kwa siri ila Mungu alimpa neema ya kuyajua mawazo ya mfalme (2 Wafalme 6:8-12). 

Hili ni jambo la msingi katika maisha ya Mkristo yaani kulijua neno la Mungu. Neno la Mungu  tukiwa nalo na likitenda kazi ndani yetu lazima tufanikiwe (Yoshua 1:8) .

Je unahitaji kuwa na imani katika neno la Mungu? Basi, ni neno la Mungu peke yake ambalo laweza kuumba imani, maana pasipo neno la Mungu hakuna imani (Waebrania 11:3 ; Warumi10:17). Ili uwe mwanafunzi wa Yesu ni lazima ulijue neno la Mungu na kulishika.(Yohana 8:31 ; Luka 2:19). Kama neno halimo ndani yetu tunayoyafanya yanakuwa hayana Mungu, hata twaweza kusalitiana. Mtu anayelitamani neno la Yesu  huling’ang’ania na kulitenda maana kwake ni nguvu. (1Wakorintho 1:18). Si kwamba Neno la Mungu ni nguvu tu: bali huleta faida (Mathayo 13:23).

Watu wengi tunapotea kwa kutokujua uwezo (nguvu) iliyomo katika neno la Mungu (Mathayo 22:29).

Yesu anasema, mtu anayelitenda neno la Mungu na kulishika huyo amepanda mbegu ambayo itazaa sana, maana ndani ya moyo wake imo mbegu ambayo ni neno la Mungu la uponyaji na mafanikio, msamaha, utu wema na mengi yanayofanana na hayo.

Yapaswa maisha yetu yawe yenye neno (mbegu) la  Mungu ili tuweze kuzaa mambo mazuri.
 

Wokovu wetu unaimarika kwenye neno la Mungu. Hilo neno la Mungu tunalipata wapi? Isaya 34:16. Upo umuhimu wa kuyachunguza maandiko ili kujua Mungu anasema nini (Matendo 17.10-11).  Je, tangu ulipowekwa msingi wa wokovu, neno limo ndani? (Hagai 2:18-19). Kila kitu kinaweza kupita lakini sio neno la Mungu (Isaya 40:8, Mathayo 24:35).
  
Ili neno litende kazi katika kinywa chako unapolitamka na kuamini ni lazima iwepo nguvu ya Roho Mtakatifu. Bila hii nguvu hamna kitakacho endelea. Utasema umeamini lakini hakutakuwa na matokeo. Mungu mwenyewe alipotamka neno liliambatana na nguvu ya Roho Mtakatifu (Mwanzo1:2-3).

**************** 

Kama una swali kuhusu somo hili nitumie barua pepe (meshackezekiakitova@gmail.com) 
au nipigie simu: 0764618028;  

Mungu akubariki


BIBLIA NI NENO LA MUNGU LILILO HAI

Katika Biblia Yako SomaZaburi 119: 9-11,105;
Waebrania 4:12;  Marko 4:21-29.

Mstari Wa KukaririKila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema           (2Tim 3:16, 17).
Baadaye Zungumzieni Jambo HiliJe, unaamini kuwa Neno la Mungu ndilo lenye mamlaka yote katika maisha?
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana TenaJitahidi kutenga muda maalum kila siku kwa ajili ya kutulia na kutafakari. Tekeleza mpango wa kusoma Biblia. Andaa alama saba za kuweka katika Biblia yako pale unapoachia kusoma ili uweze kupapata kirahisi utakapoendelea kupasoma tena wiki inayofuata.
Kazi Ya Kuandika Ya StashahadaKutoka katika 2Fal 22:8-13 na 2Fal 23:1-32 andika mageuzi yote aliyoyafanya mfalme Yosia baada ya kulisikia neno la Mungu.
Tafakari Andiko HiliMathayo 7:24-27

Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea taifa la Ujerumani.
Idadi ya watu: 80,000,000. Idadi ya Wakristo ni 75%
Ujerumani Mashariki maskini na Ujerumani Magharibi tajiri sasa zimeungana. Makanisa ya zamani yanapoteza watu. Uamsho unatakiwa haraka

1. Biblia Ni Neno La Mungu
Kwa kila mwamini neno la Mungu ni la kipekee na la thamani kubwa. Kwa karne nyingi zilizopita watu wengi wametoa maisha yao katika kuhifadhi kweli ya neno la Mungu kwa ajili yetu ili tupate kusoma. Kwa kuzingatia thamani kubwa ya neno la Mungu, na andiko kutoka Mk 4:21, swali ni hili, ‘Biblia iko wapi katika maisha yako?’ 

Je, imefichwa mbali;
Au imewekwa mahali pa juu ili ipate kumulika kila eneo la maisha yako?
2. Baraka Katika Neno La Mungu
Neno lake li hai, linanena nawe na kutenda kazi ndani yako (Ebr 4:12,13).
Neno lake ni kioo kinachokufanya ujione ulivyo kadiri unavyoendelea kulisoma. Neno lake kamwe halitakufanya ujidanganye mwenyewe, wala kuficha ukweli (Yak 1:22-24) (Mk 4:22).
Neno lake litakuandaa kikamilifu ili uwe, na ufanye kile Mungu anachotaka (2 Tim 3:15-17).

Kuanzia ulipokuwa mtoto hadi sasa umeyajua Maandiko Matakatifu yanayoweza kukupa hekima unayoihitaji kwa ajili ya kupata wokovu kwa imani katika Kristo Yesu. Maandiko yote yana pumzi ya Mungu nayanafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki, ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.

Inasemekana, na ndivyo ilivyo, kwamba Biblia ni Mwana wa Mungu katika maandishi, kwa sababu Yesu anaitwa ni Neno, na vilevile anaitwa Kweli (Yn 1:1).
Je, Unataka Kufanikiwa Na Kustawi?Basi fanya yale Yoshua aliyoagizwa kufanya (Yos 1:8). Na kama unataka kustawi kwa kila kitu zingatia Zab 1:1-3.
3. Je, Unaposoma Unasikia?
Je, umewahi kugundua kuwa unaposoma neno la Mungu ‘unasikia’ kwa ndani na si kwa masikio ya nje? Hiyo ni sauti ya Mungu. Yapasa tuwe makini na kile tunachosikia kwa sababu kwa kipimo kilekile tunachotumia, ndicho tutakachopimiwa (Mk 4:24).
4. Je, Unalitumiaje Neno La Mungu?

Unalitumia hilo neno kufanya upya moyo wako (Rum 10:17).
Unalitumia hilo neno kufanya upya mawazo yako Rum 12:2).
Unalitumia hilo neno kufanya upya maneno yako (Rum 10:10) (Mit 18:2).
Ulitumie hilo neno kufanya upya matendo yako (Yn 14:15).
Ulitumie hilo neno kuimarisha ushindi wako. Shetani hakuwa na usemi Yesu aliposema, ‘Imeandikwa’! (Mt 4:1-11)-zingatia mistari ya 4,7 na 10.
Litumie Neno Kuhuisha Maombi YakoWaamini wa kwanza mara kwa mara walinukuu maandiko ili yawaongoze katika maombi, na Mungu alijibu haraka (Mdo 4:23-31). Iwapo utaomba kwa kutumia neno la Mungu, yafuatayo yataanza kutokea:
Kwanza, unapanda mbegu ya neno.
Kisha kwa uvumilivu katika kuliomba neno, na saburihuja masuke. Na kwa kadiri unavyoendelea kuwa na imani kwa Mungu na katika neno lake, huja ngano pevu, nafaka kukomaa na hatimaye mavuno.
(Mk 4:14, 26-29) (Isa 55:10, 11) (Mwa 8:22).
Ni Muhimu Kuwapa Wengine Neno La MunguNi muhimu kwa sababu ye yote mwenye neno la Mungu anaweza kuokolewa na kupewa zaidi, mathalani: uponyaji, uhuru, uongozi, baraka na ustawi, kwa kuliamini. Lakini mtu asiye na hilo neno la Mungu ili kuliamini na kulifanyia kazi, hana baraka yo yote katika hizo zilizotajwa, na atapoteza hata hicho alichonacho, yaani maisha yake na nafsi yake milele (Mk 4:25).
5. Unapataje Kulisikia Neno?
Mungu amefanya iwe rahisi sana kuisikia sauti yake. Wewe kaa peke yako na Yeye, na kisha fungua Biblia yako. Kiri udhaifu wako na omba kujifunza kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Chukua muda kutafakari yale uliyosoma na kusikia, kwa sababu kwa njia hiyo utashangaa kuona jinsi Mungu atakavyozungumza na wewe na kujibu maswali yako.
Nikiwa mwamini mpya sikuyajua mambo haya.  Nilihudhuria kwenye kusanyiko la maombi na kimyakimya niliomba kwa ajili ya kazi yangu, nikamwombea mke wangu na watoto kwa sababu ya matatizo yote tuliyokuwa nayo. Baada ya muda mfupi nilihisi msukumo wa kuichukua Biblia yangu na ikafunguka yenyewe katika Zaburi ya 128. Na nilipoanza kusoma Mungu alinistusha na baadaye akanipooza  kwa neno lake akiuambia moyo wangu:

“Wamebarikiwa wote wamchao Bwana na kutembea katika njia zake.
Utakula matunda ya kazi yako, baraka na kustawi vitakuwa vyako.
Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, na wanao kama matawi ya mtende mezani pako”.
Naliliamini neno la Mungu na leo hii, baada ya miaka kadhaa kupita naweza kuona jinsi Mungu alivyoitunza ahadi yake kwa kuibariki familia yangu na kazi yangu.
6. Namna Ya Kufurahia Usomaji Wa Biblia
Watu wengi huanza na kitabu cha Mwanzo na baadaye huacha wanapokutana na sehemu ngumu katika Agano la Kale ambazo hawazielewi. Sisi sote tunapenda kula vyakula mbalimbali siku kwa siku, na hivyo ndivyo ilivyo hata kwa chakula cha kiroho. Jaribu kufuata mpangilio ufuatao nawe utapata mlo tofauti kila siku. Kila siku soma Zaburi za kuabudu na Mithali kwa ajili ya kupata hekima.

Jumatatu
Hadithi za watu mashuhuri na za historia ya Biblia. Anza na kitabu cha Mwanzo na kuendelea hadi kitabu cha Esta.
Jumanne
Taarifa za watu waliomjua Yesu vizuri. Anza na injili ya Mathayo  na kuendelea hadi ya Luka.
Jumatano
Tembea katika vilima na mabonde ya ushairi. Anza na kitabu cha Ayubu  hadi Wimbo Ulio Bora.
Alhamisi
Nyaraka za upendo kutoka kwa Yohana. Anza na injili yake, ikifuatiwa na nyaraka zake, na kuishia na Ufunuo wake.
Ijumaa
Unabii wa Biblia. Anza na Isaya na kuendelea hadi Malaki; utastaajabu.
Jumamosi
Nyaraka kutoka kwa watu mashuhuri wa Mungu. Anza na Warumi, endelea hadi Petro na Yuda.
Jumapili
Tembelea makanisa yaliyo hai na misheni zilizoko mstari wa mbele kwa kusoma kitabu cha Matendo ya Mitume.
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Huu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina
  

UWEZA WA JINA LA YESU

Mtume Paulo anasema katika Waraka wake kwa Wakolosai sura ya tatu na mstari wa kumi na saba kuwa; “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika JINA LA BWANA YESU, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.”
            Hii ina maana ya kuwa, tukila tule katika Jina la Yesu Kristo. Tukilala tulale katika Jina la Yesu Kristo. Tukizungumza tuzungumze katika jina la Yesu Kristo. Tukiimba tuimbe katika jina la Yesu Kristo. Tukitembea tutembee katika jina la Yesu Kristo. Tukisafiri tusafiri katika jina la Yesu Kristo. Tukilima shambani tulime katika jina la Yesu Kristo; na kadhalika.
            Kwa nini tunatakiwa tufanye mambo yote katika jina la Yesu Kristo? Jina hili la Yesu Kristo lina sehemu gani katika maisha yetu ya kila siku?
Kama tunatakiwa kufanya mambo yote katika jina la Yesu Kristo, kwa nini hatufanyi hivyo?
Ukitafakari maagizo tuliyopewa katika biblia utaona ya kuwa, maisha yetu yote yanalitegemea jina hili la Yesu Kristo.
Kama mambo yetu yote yanatakiwa yafanyike kwa jina la Yesu, basi ni muhimu tujifunze zaidi na zaidi kila siku juu ya jina hili la ajabu.
Ni maombi yangu kwa Mungu Baba, katika jina la Yesu Kristo ya kuwa maneno yaliyomo katika somo hili yatachochea kwa upya kiu iliyomo ndani yako ya kutaka kufahamu zaidi siri iliyomo ndani ya jina la Yesu Kristo.

Je, biblia kweli ni neno la Mungu?

wali: "Je, biblia kweli ni neno la Mungu?"

Jibu: 
Jibu letu katika swali hili halitagusia tu mtazamo wetu juu ya biblia na umuhimu wake maishani mwetu bali pia hatimaye litakuwa na mguso wa milele maishani mwetu. Kama biblia kweli ni neno la Mungu, basi natulifurahie, tulisome, tulitii na kuliamini. Kama biblia ni neno la Mungu basi kulikataa ni kumkataa Mungu.

Kupatiwa kwetu biblia na Mungu ni kithibitisho cha kuwa Mungu anatupenda. Neno “ufunuo” lina maana ya kuwa Mungu aliwasiliana na mwanadamu jinsi alivyo na ni kwa jinsi gani tunaweza kupata ushirika mwema naye. Haya ni mambo ambayo hatungeweza kuyajua kama Mungu hangekuwa ameyawasilisha kwetu katika biblia. Ijapokuwa ufunuo wa Mungu katika biblia umetolewa kwa mfululizo ndani ya takriban miaka 1500 umehifadhi kila kitu mwanadamu anahitaji kumjua Mungu ili awe na ushirika mwema naye. Kama biblia ni neno la Mungu kweli basi ndiyo mamlaka ya mwisho katika mambo ya kiimani, dini na wema.

Swali ambalo sharti tujiulize ni tunawezaje kujua bibilia ni neno la Mungu wala si kitabu tu? Ni kitu gani maaluum ndani ya biblia ambacho huifanya biblia iwe kitabu maalum mbali na vitabu vyengine vya dini Je, kuna ushahidi kuwa biblia ni neno la Mungu kweli? Haya ndiyo baadhi ya maswali ambayo yanahitajika kuangaliwa kama ni tunahitaji kujua kweli biblia ni neno al Mungu, lilitoka kwake na lenye kujitosheleza katika mambo yote ya kiimani.

Hakuwezi kuwa na shaka katika swala la kuwa biblia ni neno la Mungu. Haya yanapatikana katika aya kama Timotheo wa pili 3:15-17, inayosema, “… Kutoka utotoni mmeyajua maandiko matakatifu, yenye uwezo wa kuwafanya ninyi werevu kwa ajili ya wokovu kupitia imani iliyo katika Kristo Yesu. Maandiko yote yametolewa kwa pumzi ya Mungu na yanafaa kwa mafundisho, kwa kuonya, kwa kurekebisha, kwa kuelekeza katika hakii ili mtu wa Mungu akamilishwe kwa ajili ya kila kazi njema.”

Ili tuyajibu maswali haya kwa usahihi, lazima tutazame ushahidi wa ndani na nje wa kuwa kweli biblia ni neno la Mungu. Ushahidi wa ndani ya biblia ni yale maandiko ambayo yanaelezea kuhusu chanzo cha kuweko kwake. Ushahdi wa kwanza ni katika ule umoja wake biblia. Ingawa ina vitabu sitini na sita vilivyoandikwa katika mabara matatu kwa lugha tatu tofauti ndani ya takriban miaka 1500 na waandishi zaidi ya 40 (waliotoka katika taaluma mbalimbali), biblia inabaki kitabu chenye kuhifadhi umoja kutoka mwanzo mpaka mwisho bila kujipinga chenyewe. Hali hii ni maalum kulinganisha na vitabu vyengine na inathibitisha kuweko kwa sauti ya Mungu ikinakiliwa na wanadamu.

Lengine katika ushahidi wa ndani, lapatikana katika unabii ulioorodheshwa ndani ya kurasa za biblia. Humu tunapata unabii juu ya mataifa binafsi kama vile Israeli, unabii wa miji Fulani, unabii wa maisha ya wanadamu na hata wa kuja kwake masihi, mwokozi si wa Israeli tu bali hata kwa wale pia watakaomwamini. kinyume cha unabii unaopatikana katika vitabu vyengine ama ule uliofanywa na Nostradamus, unabii wa kibiblia unatimia. Kuna unabii zaidi ya mia tatu kuhusu Yesu kristo katika Agano la kale pekee. Haikutabiriwa tu atazaliwa wapi na atakuwa wa jamii gani lakini pia ya kuwa angekufa na kufufuka siku ya tatu. Hakuna njia mwafaka ya kuelezea ni kwa uwezo gani unabii huu ulitimizwa ispokuwa kukiri ni kwa uwezo wa Mungu. Hakuna kitabu chenginecha dini chenye unabii unaodhihirika kama Biblia.

Ushahidi wa tatu unapatikana katika uweza na mamlaka ya Biblia. Hili si jambo dogo la kupuuzwa. Biblia ina mamlaka kuliko vitabu vyovyote vyengine. Uwezo huu unaonekana katika maisha ya wanadamu kama vile watu wasiohesabika wameweza kubadilishwa kwa kusoma biblia. Wenye kutumia mihadharati wameponywa na biblia, wahalifu sugu pia wamebadilishwa na biblia, wenye dhambi hukaripiwa na biblia na chuki kubadilishwa kuwa upendo kwa kulisoma biblia. Biblia ina uwezo wa kubadilisha maisha ya mtu kwa kuwa ni neno la Mungu.

Mbali na ushahidi wa ndani ya biblia, kuna ushahidi wa nje ya biblia unaothibitisha kuwa biblia kweli ni neno la Mungu. Umakini wa historia kama inavyoelezewa katika biblia ni ushahidi pia. Kupitia watafiti wa mabaki ya vitu vya kale na vitabu vyengine vilivyoandikwa, ratiba ya kihistoria katika biblia imehakikishwa mara kwa mara kuwa ya kweli. Watafiti hao pamoja na majarida wanayoyaandika husema ya kwamba biblia ndicho kitabu chenye kuongoza vyema katika historia sahihi ya maeneo mbalimbali. Jinsi biblia ilivyohifadhi histiria sahihi ya vizazi mbalimbali ni thibitisho ya kuwa ni kitabu cha ukweli pia katika kushughulikia maswala ya dini na mafundisho yake. Hili pia huthibitisha ya kuwa hili kweli ni neno la Mungu.

Jambo lengine ni kwamba heshima ya waandishi wa habari hizi za biblia. Mungu aliwatumia watu wa tabaka mbalimbali kuandika habari hizi. Tukuchunguza maisha ya watu hawa na ya kwamba walikuwa tayari hata kufa kwa ajili ya uaminifu wao kwa Mungu kwa ajili ya yale waiyoyaamini; Inathibitisha kuwa, watu hawa wanyonge na waaminifu walikuwa na uhakika kwamba Mungu kweli alikuwa amezungumza nao. Wale waliondika agano jipya na mamia ya waumini wengine (Wakorintho wa kwanza 15:6) walijua ukweli wa ujumbe wao kwa kuwa walikuwa wamemuona na kushirikiana na Yesu kristo baada ya kufa. Mabadiliko ya kumuona kristo aliyefufuka yalipokewa na uzito mkuu na watu hawa. Walibadilika kutoka kwa uoga wa kujificha na kuwa watu ambao hawaogopi kufa kwa ajili ya ujumbe wa Mungu uliokuwa umefunuliwa kwao. Maisha yao na vifo vyao vinathibitisha ya kwamba kweli biblia ni Neno la Mungu.

Ushahidi mwengine ni katika ile hali ya kutokuharibiwa kwa biblia. Kwa sababu ya umuhimu wake na kwamba ni neno la Mungu, biblia imepitia mapambano hatari mengi katika majaribio ya kuliharibu biblia kuliko kitabu chochote chengine katika historia Kutoka watawala wa jadi wa kirumi kama Diocletian, kupitia madikteta wa kikomiunisti na wale wasioamini kuna Mungu wanaoisho siku hizi, biblia imedhibiti hali yake na kudumu zaidi ya wapinzani wake. Hata sasa ndicho kitabu kinachochapishwa kwa wingi duniani.

Vizazi vyote na nyakati zote duniani,wapinzani wamekuwa wakipuuza biblia na kusema ni hadithi tu za watu lakini watafiti wa kihitoria wadumu wakithibitisha ya kuwa biblia ni kitabu cha kweli. Pia wapinzani wake wameshutumu mafundisho yake kuwa ya kijadi nayaliyopitwa na wakati lakini wema wake na mfumo wake wa kisheria umekubalika katika jamii na mila mbalimbali duniani kote. Inaendelea kushambuliwa na sayansi, saikologia, na vyama vya kisiasa na bado biblia inabaki na umuhimu sawa na ule iliyokuwa nao wakati ikiandikwa. Ni kitabu kilichobadilisha maisj\ha na tamaduni kwa muda wote wa miaka 2000 iliyopita. Haijalishi wapinzani wake wanapambana ki vipi, biblia inabaki ikiwa ni kitabu chenye nguvu, kweli na umuhimu sawa na ule kilichokuwa nao kabla kupigwa vita. Kuhifadhika kwa hali yake ya asili hata baada ya mashambulizi haya yote ni ishara ya kuwa biblia ni neno la Mungu. Isitushangaze ile hali ya kuwa bilia inapigwa vita na kuibuka bado mshindi bila madhara yoyote. Kumbuka Yesu alisema, “ Mbingu na dunia vitapita, lakini neno langu halitapita kamwe” (Marko 13:31). Baada ya kupitia ushahidi huu mtu bila shaka anaweza kusema “kweli Biblia ni Neno la Mungu.”

Tuwe makini, ndoa si jambo la mchezo!!


Katika maisha ya mwanadamu, kuna mambo mawili yaliyo muhimu zaidi. La kwanza ni uamuzi wa kumfuataYesu na la pili ni uamuzi wa kuoa. Tafakari, kuoa si sawa na kununua shati. Ukilichoka na shati unaweza kununua nyingine lakini, huwezi kumwacha mke wako hata kama ukimchoka. Neno la Mungu linatuonya hatari ya kuoa mwanamke asiye mchaji wa Mungu; Twasoma: “Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi” (Mithali. 21:19). “Kutonatona daima siku ya mvua nyingi, na mwanamke mgomvi ni sawasawa; 16atakaye kumzuia huyo huuzuia upepo” (Mithali. 27:15-16). Zingatia: Pengine mtu atasema, “mchumba wangu ana imani tofauti, walakini tukioana nitamfundisha.”Lakini ikumbukwe mara nyingi, baada ya kufunga ndoa, watu hubadilika asitake kufundishwa tena.Tukumbuke mfalme Sulemani alikuwa na hekima kuliko wanadamu wote. Walakini, alipata hasara kubwa kwa sababu aliwapenda wanawake wageni wasio mcha Mungu na matokeo yake badala ya kuwafundisha imani yake, “yeye mwenyewe alinaswa na imani yao” (1Wafalme 11:1-4). Basi tujiulize, je sisi tunayo hekima kuliko Sulemani? Ni bora mtu amfundishe mchumba kabla hawajaoana na kuhakikisha kuwa ameamua kumfuata Bwana kwa moyo wake wote na si kwa sababu ya ndoa, ndipo atakapokuwa na amani na furaha katika ndoa yake. Tukumbuke faida moja wapo ya kuoa katika katisa ni kupata mke alifundishwa maadili na wanawake waliomtangulia; Twasoma: “Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wautakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema; ili wawatie – wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na uwapenda watoto wao; na kuwa wenye kiasi, kuwa safi,kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe, ili neno la Mungu lisitukanwe” (Tit. 2:3-5). Hivyo ni dhahiri kuna faida kwa mkristo kujipatia mke aliyefunzwa maadili ya ndani ya kanisa. Zingatia: Kuna baadhi ya watu wamevutwa sana na maumbile au mambo ya kimwili ya wachumba wao lakini Biblia inatukumbusha kuchunguza mioyo yao zaidi kuliko sura ya nje; Tasoma: “Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa” (Mithali. 31:30). “Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana” (Mithali 19:14). Je unazijua sifa za mke mwema? Mungu ameeleza peupe; Soma: (Mithali 31:10-31)
HATARI YA KUOANA NA ASIYE MCHAJI WA MUNGU
Kama tulivyojifunza hako juu hatari moja wapo ya kuoana na wasio wachaji wa Mungu ni kuishia kuvutwa na upotofu na kuanguka kiimani; Twasoma:”Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye atakuangamiza upesi” (Kumbukumbu 7:4). Na hayo ndiyo yaliyomapata Suleima kama tulikwisha kuoona; Soma tena: (1 Wafalme 11:1-4) Tukumbuke ikiwa tutaanguka katika uovu, mwisho wake utakuwa ni kutupwa katika hukumu (adhabu ya milele); Twasoma: “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uachafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui,ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayo fanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Galatia 5:19-21) “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauwaji, na wazizi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili” (Ufunuo 21:8) “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani hilo ziwa la moto. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:14- 15) Zingatia: Ndoa ni kifungo hivyo tukumbuke tunapoana hatuna ruhusa ya kuacha hata kama wenzi wetu ni wabaya vipi; Twasoma: “Lakini wale waliokwisha kuoana nawagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; lakini ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.” (1 Wakorintho 7:10-11) “Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumwe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu.” (1 Wakorintho 7:39)
Hivyo ni dhahiri tunaaswa kuwa makini tunapo wachagua wenzi wetu, tukikumbuka ya kuwa kifungo cha
ndoa ni mpaka kifo