Labels

Sunday, May 18, 2014

UWEZA WA NENO LA MUNGU/power of word of God

po umuhimu wa kujua neno la Mungu katika maisha ya Mkristo halisi.
 
Biblia  inatuambia Yesu Kristo ndiye Neno la Mungu. Kwa maneno mengine Yesu ndiye Neno ambalo Mkristo anapaswa kuwa nalo (Yohana 1:1).

Kwa kusema hivyo kuna  umuhimu wa kumjua Yesu na kumshika, kwa maana yeye ndiye Neno la Mungu. Katika Biblia mtume Petro anasema mbele za Yesu kwamba, twende kwa nani na wewe ndio mwenye maneno ya uzima? Petro alijua upo umuhimu wa kumjua Yesu kama Neno maana ndani ya Neno kuna uzima
Biblia inasema neno la Kristo likae kwa wingi ndani yetu (Wakolosai 3:16).
Kwa nini basi neno la Kristo likae kwa wingi ndani yetu? Ni kwa sababu lina mambo yafuatayo ambayo ni muhimu katika maisha yetu ya Ukristo. Mambo hayo ni…
A) Neno la Mungu li Hai
B) Neno la Mungu lina nguvu (Mwanzo 1:6).
C) Neno la Mungu lina ukali kuliko upanga
D) Neno la Mungu linachoma hata kuzigawanya nafsi, roho viungo na mafuta yaliyomo ndani yake
E) Neno la Mungu li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo


KWA NINI NENO LA MUNGU LI HAI?
Neno la Mungu li hai kwa sababu  Mungu mwenyewe analithibitisha kwamba li hai maana 
a) Linafanya mabadiliko (Isaya 55:10-11).
b) Linatupa kushinda dhambi (Zaburi 119:11).
c) Neno la Mungu  li hai kwa sababu linatupa mafanikio katik mwili. Petro anasema ”kwa neno lako tunatupa nyavu zetu.“  Hapa tunaona kuwa Neno la Mungu  pekee yake ndilo linaloweza kuleta majibu katika maisha yetu (Luka 5:3-6).


Uhai wa Neno la Mungu kwa mtu ndio unaoleta kushinda dhambi. Nao wakamshinda kwa neno la ushuhuda wao (Ufunuo 12:11).

Daudi aligundua au kwa maneno mengine alifahamu umuhimu wa neno la Mungu katika maisha, kama vile mtume Paulo anavyosema na Wakolosai kwa habari ya neno la Kristo kwamba likae kwa wingi ndani ya mioyo yetu

Neno la Mungu lina nguvu na ndio maana  tunamshinda  shetani kwa neno la Mungu.
Yesu kama kielelezo yeye mwenyewe ni neno ndani ya neno anamshinda shetani (Luka 4:1-12). 


Katika mistari hiyo tunaona Yesu anamwambia  shetani  ”imeandikwa“   Shetani nae anageuza usemi nae anamwambia Yesu ”imeandikwa kwamba atakuagizia malaika usije ukajikwaa mguu wako.“ Kwa kuwaYesu neno la Mungu limo ndani yake hamwambii tena shetani imeandikwa ila anamwambia imenenwa. Kwa maneno mengine tukiwa na neno la Yesu ndani yetu hatuwezi kuyumbishwa. Kwanini? Kwa sababu tumeshaona jinsi ambavyo shetani  anajaribu kutumia neno la Mungu   kwa kusema ”imeandikwa.“  Na ni kweli imeandikwa ananukuu kutoka kitabu cha Zaburi 91 :1-12. Hata kama shetani ananukuu maandiko haina sababu  yamimi kushindwa na shetani  maana Yesu tayari alikwisha mshinda. Yesu kumshinda shetani ina nipelekea mimi kusoma neno la Mungu kwa bidiisana. Kwa mfano, ni kweli kabisa imeandikwa mtakula vitu vya kufisha havitawadhuru lakini je, ninywe sumu sitakufa kwa sababu imeandikwa? Hapana, ukinywa hakika utakufa. Shetani hutumia mandiko kuwafunga wasiojua neno la KristoYesu. 

Katika Biblia tunasoma pia kwamba ”imeandikwa“ Wanandoa MKE na MUME wasinyimane. Kwa kutojua neno vijana wa kiume na wa kike wamedanganywa. Si hao tu hata walioko kwenye ndoa wametegwa kwa andiko hilo. Neno linasema katika Mithali 6:32 ”Aziniye na mwanamke hana akili kabisa“ na Mwanamke vivyo hivyo akizini na mwanaume hana akili kabisa. Watu wamepata hasara ya mambo mengi kwa kutojua neno la Mungu. Ili tuweze kumshinda shetani  ni lazima  neno la Yesu liwe ndani  yetu ndiposa tutamshinda shetani. Ayubu kwa neno la Mungu alishinda. (Ayubu 19:25-27, Waefeso 6:17).

Nataka nikwambie neno la Mungu ni msaada katika maisha yetu maana hutupa  majibu ya maisha yetu. Katika Luka 5:3-6 tunasoma jinsi Petro na wenzake walivyopata samaki wengi kwa kutii neno la Kristo. Kumbuka pia juu ya yule akida, alimwambia Yesu ”...sema neno tu na mtumwa wangu atapona“ (Luka 7:2-10). Yesu akisema neno lazima mabadiliko yatokee. 

Neno la Mungu lina ukali kuliko upanga. Kwa nini neno la Mungu  lina ukali kuliko upanga? Upanga unaweza kukukata na usipone. Lakini neno linakata na kuponya. Kwa neno hili wafalme wanatubu. Yona alitumia neno la Mungu likawa kali watu wakatubu. (Yona 3:1-10; Matendo ya Mitume 8:18-24).

Neno la Mungu linachoma hata kuzigawa nafsi na roho na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake (Matendo 7:51-54, Yohana 4:16 -18, 27-29). Mwanamke akaambiwa mambo yake; Neno likachambua kila tabia..

Neno la Mungu li jepesi kutambua mawazo na makusudi ya moyo.
Yesu kama Neno la Mungu anajua mambo ambayo watu wanawaza ndani ya mioyo yao (Luka 5:17-24, 6:6-8 ; Mathayo 16:1-4)Yapo makusudi ya moyo ambayo ni ya siri sana kwa mwanadamu lakini nataka nikuambie neno la  Mungu ni jepesi kutambua makusudi ya moyo. 


Mtume Petro aliyependa kujua neno la Mungu, naye pia Mungu alimjalia neema ya kuyajua makusudi ya moyo wa mwanadamu (Matendo 5:1-11). Elisha aliyajua makusudi ya moyo wa mfalme ya kuwatenda Israeli kwa siri ila Mungu alimpa neema ya kuyajua mawazo ya mfalme (2 Wafalme 6:8-12). 

Hili ni jambo la msingi katika maisha ya Mkristo yaani kulijua neno la Mungu. Neno la Mungu  tukiwa nalo na likitenda kazi ndani yetu lazima tufanikiwe (Yoshua 1:8) .

Je unahitaji kuwa na imani katika neno la Mungu? Basi, ni neno la Mungu peke yake ambalo laweza kuumba imani, maana pasipo neno la Mungu hakuna imani (Waebrania 11:3 ; Warumi10:17). Ili uwe mwanafunzi wa Yesu ni lazima ulijue neno la Mungu na kulishika.(Yohana 8:31 ; Luka 2:19). Kama neno halimo ndani yetu tunayoyafanya yanakuwa hayana Mungu, hata twaweza kusalitiana. Mtu anayelitamani neno la Yesu  huling’ang’ania na kulitenda maana kwake ni nguvu. (1Wakorintho 1:18). Si kwamba Neno la Mungu ni nguvu tu: bali huleta faida (Mathayo 13:23).

Watu wengi tunapotea kwa kutokujua uwezo (nguvu) iliyomo katika neno la Mungu (Mathayo 22:29).

Yesu anasema, mtu anayelitenda neno la Mungu na kulishika huyo amepanda mbegu ambayo itazaa sana, maana ndani ya moyo wake imo mbegu ambayo ni neno la Mungu la uponyaji na mafanikio, msamaha, utu wema na mengi yanayofanana na hayo.

Yapaswa maisha yetu yawe yenye neno (mbegu) la  Mungu ili tuweze kuzaa mambo mazuri.
 

Wokovu wetu unaimarika kwenye neno la Mungu. Hilo neno la Mungu tunalipata wapi? Isaya 34:16. Upo umuhimu wa kuyachunguza maandiko ili kujua Mungu anasema nini (Matendo 17.10-11).  Je, tangu ulipowekwa msingi wa wokovu, neno limo ndani? (Hagai 2:18-19). Kila kitu kinaweza kupita lakini sio neno la Mungu (Isaya 40:8, Mathayo 24:35).
  
Ili neno litende kazi katika kinywa chako unapolitamka na kuamini ni lazima iwepo nguvu ya Roho Mtakatifu. Bila hii nguvu hamna kitakacho endelea. Utasema umeamini lakini hakutakuwa na matokeo. Mungu mwenyewe alipotamka neno liliambatana na nguvu ya Roho Mtakatifu (Mwanzo1:2-3).

**************** 

Kama una swali kuhusu somo hili nitumie barua pepe (meshackezekiakitova@gmail.com) 
au nipigie simu: 0764618028;  

Mungu akubariki


BIBLIA NI NENO LA MUNGU LILILO HAI

Katika Biblia Yako SomaZaburi 119: 9-11,105;
Waebrania 4:12;  Marko 4:21-29.

Mstari Wa KukaririKila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema           (2Tim 3:16, 17).
Baadaye Zungumzieni Jambo HiliJe, unaamini kuwa Neno la Mungu ndilo lenye mamlaka yote katika maisha?
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana TenaJitahidi kutenga muda maalum kila siku kwa ajili ya kutulia na kutafakari. Tekeleza mpango wa kusoma Biblia. Andaa alama saba za kuweka katika Biblia yako pale unapoachia kusoma ili uweze kupapata kirahisi utakapoendelea kupasoma tena wiki inayofuata.
Kazi Ya Kuandika Ya StashahadaKutoka katika 2Fal 22:8-13 na 2Fal 23:1-32 andika mageuzi yote aliyoyafanya mfalme Yosia baada ya kulisikia neno la Mungu.
Tafakari Andiko HiliMathayo 7:24-27

Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea taifa la Ujerumani.
Idadi ya watu: 80,000,000. Idadi ya Wakristo ni 75%
Ujerumani Mashariki maskini na Ujerumani Magharibi tajiri sasa zimeungana. Makanisa ya zamani yanapoteza watu. Uamsho unatakiwa haraka

1. Biblia Ni Neno La Mungu
Kwa kila mwamini neno la Mungu ni la kipekee na la thamani kubwa. Kwa karne nyingi zilizopita watu wengi wametoa maisha yao katika kuhifadhi kweli ya neno la Mungu kwa ajili yetu ili tupate kusoma. Kwa kuzingatia thamani kubwa ya neno la Mungu, na andiko kutoka Mk 4:21, swali ni hili, ‘Biblia iko wapi katika maisha yako?’ 

Je, imefichwa mbali;
Au imewekwa mahali pa juu ili ipate kumulika kila eneo la maisha yako?
2. Baraka Katika Neno La Mungu
Neno lake li hai, linanena nawe na kutenda kazi ndani yako (Ebr 4:12,13).
Neno lake ni kioo kinachokufanya ujione ulivyo kadiri unavyoendelea kulisoma. Neno lake kamwe halitakufanya ujidanganye mwenyewe, wala kuficha ukweli (Yak 1:22-24) (Mk 4:22).
Neno lake litakuandaa kikamilifu ili uwe, na ufanye kile Mungu anachotaka (2 Tim 3:15-17).

Kuanzia ulipokuwa mtoto hadi sasa umeyajua Maandiko Matakatifu yanayoweza kukupa hekima unayoihitaji kwa ajili ya kupata wokovu kwa imani katika Kristo Yesu. Maandiko yote yana pumzi ya Mungu nayanafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki, ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.

Inasemekana, na ndivyo ilivyo, kwamba Biblia ni Mwana wa Mungu katika maandishi, kwa sababu Yesu anaitwa ni Neno, na vilevile anaitwa Kweli (Yn 1:1).
Je, Unataka Kufanikiwa Na Kustawi?Basi fanya yale Yoshua aliyoagizwa kufanya (Yos 1:8). Na kama unataka kustawi kwa kila kitu zingatia Zab 1:1-3.
3. Je, Unaposoma Unasikia?
Je, umewahi kugundua kuwa unaposoma neno la Mungu ‘unasikia’ kwa ndani na si kwa masikio ya nje? Hiyo ni sauti ya Mungu. Yapasa tuwe makini na kile tunachosikia kwa sababu kwa kipimo kilekile tunachotumia, ndicho tutakachopimiwa (Mk 4:24).
4. Je, Unalitumiaje Neno La Mungu?

Unalitumia hilo neno kufanya upya moyo wako (Rum 10:17).
Unalitumia hilo neno kufanya upya mawazo yako Rum 12:2).
Unalitumia hilo neno kufanya upya maneno yako (Rum 10:10) (Mit 18:2).
Ulitumie hilo neno kufanya upya matendo yako (Yn 14:15).
Ulitumie hilo neno kuimarisha ushindi wako. Shetani hakuwa na usemi Yesu aliposema, ‘Imeandikwa’! (Mt 4:1-11)-zingatia mistari ya 4,7 na 10.
Litumie Neno Kuhuisha Maombi YakoWaamini wa kwanza mara kwa mara walinukuu maandiko ili yawaongoze katika maombi, na Mungu alijibu haraka (Mdo 4:23-31). Iwapo utaomba kwa kutumia neno la Mungu, yafuatayo yataanza kutokea:
Kwanza, unapanda mbegu ya neno.
Kisha kwa uvumilivu katika kuliomba neno, na saburihuja masuke. Na kwa kadiri unavyoendelea kuwa na imani kwa Mungu na katika neno lake, huja ngano pevu, nafaka kukomaa na hatimaye mavuno.
(Mk 4:14, 26-29) (Isa 55:10, 11) (Mwa 8:22).
Ni Muhimu Kuwapa Wengine Neno La MunguNi muhimu kwa sababu ye yote mwenye neno la Mungu anaweza kuokolewa na kupewa zaidi, mathalani: uponyaji, uhuru, uongozi, baraka na ustawi, kwa kuliamini. Lakini mtu asiye na hilo neno la Mungu ili kuliamini na kulifanyia kazi, hana baraka yo yote katika hizo zilizotajwa, na atapoteza hata hicho alichonacho, yaani maisha yake na nafsi yake milele (Mk 4:25).
5. Unapataje Kulisikia Neno?
Mungu amefanya iwe rahisi sana kuisikia sauti yake. Wewe kaa peke yako na Yeye, na kisha fungua Biblia yako. Kiri udhaifu wako na omba kujifunza kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Chukua muda kutafakari yale uliyosoma na kusikia, kwa sababu kwa njia hiyo utashangaa kuona jinsi Mungu atakavyozungumza na wewe na kujibu maswali yako.
Nikiwa mwamini mpya sikuyajua mambo haya.  Nilihudhuria kwenye kusanyiko la maombi na kimyakimya niliomba kwa ajili ya kazi yangu, nikamwombea mke wangu na watoto kwa sababu ya matatizo yote tuliyokuwa nayo. Baada ya muda mfupi nilihisi msukumo wa kuichukua Biblia yangu na ikafunguka yenyewe katika Zaburi ya 128. Na nilipoanza kusoma Mungu alinistusha na baadaye akanipooza  kwa neno lake akiuambia moyo wangu:

“Wamebarikiwa wote wamchao Bwana na kutembea katika njia zake.
Utakula matunda ya kazi yako, baraka na kustawi vitakuwa vyako.
Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, na wanao kama matawi ya mtende mezani pako”.
Naliliamini neno la Mungu na leo hii, baada ya miaka kadhaa kupita naweza kuona jinsi Mungu alivyoitunza ahadi yake kwa kuibariki familia yangu na kazi yangu.
6. Namna Ya Kufurahia Usomaji Wa Biblia
Watu wengi huanza na kitabu cha Mwanzo na baadaye huacha wanapokutana na sehemu ngumu katika Agano la Kale ambazo hawazielewi. Sisi sote tunapenda kula vyakula mbalimbali siku kwa siku, na hivyo ndivyo ilivyo hata kwa chakula cha kiroho. Jaribu kufuata mpangilio ufuatao nawe utapata mlo tofauti kila siku. Kila siku soma Zaburi za kuabudu na Mithali kwa ajili ya kupata hekima.

Jumatatu
Hadithi za watu mashuhuri na za historia ya Biblia. Anza na kitabu cha Mwanzo na kuendelea hadi kitabu cha Esta.
Jumanne
Taarifa za watu waliomjua Yesu vizuri. Anza na injili ya Mathayo  na kuendelea hadi ya Luka.
Jumatano
Tembea katika vilima na mabonde ya ushairi. Anza na kitabu cha Ayubu  hadi Wimbo Ulio Bora.
Alhamisi
Nyaraka za upendo kutoka kwa Yohana. Anza na injili yake, ikifuatiwa na nyaraka zake, na kuishia na Ufunuo wake.
Ijumaa
Unabii wa Biblia. Anza na Isaya na kuendelea hadi Malaki; utastaajabu.
Jumamosi
Nyaraka kutoka kwa watu mashuhuri wa Mungu. Anza na Warumi, endelea hadi Petro na Yuda.
Jumapili
Tembelea makanisa yaliyo hai na misheni zilizoko mstari wa mbele kwa kusoma kitabu cha Matendo ya Mitume.
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Huu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina
  

UWEZA WA JINA LA YESU

Mtume Paulo anasema katika Waraka wake kwa Wakolosai sura ya tatu na mstari wa kumi na saba kuwa; “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika JINA LA BWANA YESU, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.”
            Hii ina maana ya kuwa, tukila tule katika Jina la Yesu Kristo. Tukilala tulale katika Jina la Yesu Kristo. Tukizungumza tuzungumze katika jina la Yesu Kristo. Tukiimba tuimbe katika jina la Yesu Kristo. Tukitembea tutembee katika jina la Yesu Kristo. Tukisafiri tusafiri katika jina la Yesu Kristo. Tukilima shambani tulime katika jina la Yesu Kristo; na kadhalika.
            Kwa nini tunatakiwa tufanye mambo yote katika jina la Yesu Kristo? Jina hili la Yesu Kristo lina sehemu gani katika maisha yetu ya kila siku?
Kama tunatakiwa kufanya mambo yote katika jina la Yesu Kristo, kwa nini hatufanyi hivyo?
Ukitafakari maagizo tuliyopewa katika biblia utaona ya kuwa, maisha yetu yote yanalitegemea jina hili la Yesu Kristo.
Kama mambo yetu yote yanatakiwa yafanyike kwa jina la Yesu, basi ni muhimu tujifunze zaidi na zaidi kila siku juu ya jina hili la ajabu.
Ni maombi yangu kwa Mungu Baba, katika jina la Yesu Kristo ya kuwa maneno yaliyomo katika somo hili yatachochea kwa upya kiu iliyomo ndani yako ya kutaka kufahamu zaidi siri iliyomo ndani ya jina la Yesu Kristo.

Je, biblia kweli ni neno la Mungu?

wali: "Je, biblia kweli ni neno la Mungu?"

Jibu: 
Jibu letu katika swali hili halitagusia tu mtazamo wetu juu ya biblia na umuhimu wake maishani mwetu bali pia hatimaye litakuwa na mguso wa milele maishani mwetu. Kama biblia kweli ni neno la Mungu, basi natulifurahie, tulisome, tulitii na kuliamini. Kama biblia ni neno la Mungu basi kulikataa ni kumkataa Mungu.

Kupatiwa kwetu biblia na Mungu ni kithibitisho cha kuwa Mungu anatupenda. Neno “ufunuo” lina maana ya kuwa Mungu aliwasiliana na mwanadamu jinsi alivyo na ni kwa jinsi gani tunaweza kupata ushirika mwema naye. Haya ni mambo ambayo hatungeweza kuyajua kama Mungu hangekuwa ameyawasilisha kwetu katika biblia. Ijapokuwa ufunuo wa Mungu katika biblia umetolewa kwa mfululizo ndani ya takriban miaka 1500 umehifadhi kila kitu mwanadamu anahitaji kumjua Mungu ili awe na ushirika mwema naye. Kama biblia ni neno la Mungu kweli basi ndiyo mamlaka ya mwisho katika mambo ya kiimani, dini na wema.

Swali ambalo sharti tujiulize ni tunawezaje kujua bibilia ni neno la Mungu wala si kitabu tu? Ni kitu gani maaluum ndani ya biblia ambacho huifanya biblia iwe kitabu maalum mbali na vitabu vyengine vya dini Je, kuna ushahidi kuwa biblia ni neno la Mungu kweli? Haya ndiyo baadhi ya maswali ambayo yanahitajika kuangaliwa kama ni tunahitaji kujua kweli biblia ni neno al Mungu, lilitoka kwake na lenye kujitosheleza katika mambo yote ya kiimani.

Hakuwezi kuwa na shaka katika swala la kuwa biblia ni neno la Mungu. Haya yanapatikana katika aya kama Timotheo wa pili 3:15-17, inayosema, “… Kutoka utotoni mmeyajua maandiko matakatifu, yenye uwezo wa kuwafanya ninyi werevu kwa ajili ya wokovu kupitia imani iliyo katika Kristo Yesu. Maandiko yote yametolewa kwa pumzi ya Mungu na yanafaa kwa mafundisho, kwa kuonya, kwa kurekebisha, kwa kuelekeza katika hakii ili mtu wa Mungu akamilishwe kwa ajili ya kila kazi njema.”

Ili tuyajibu maswali haya kwa usahihi, lazima tutazame ushahidi wa ndani na nje wa kuwa kweli biblia ni neno la Mungu. Ushahidi wa ndani ya biblia ni yale maandiko ambayo yanaelezea kuhusu chanzo cha kuweko kwake. Ushahdi wa kwanza ni katika ule umoja wake biblia. Ingawa ina vitabu sitini na sita vilivyoandikwa katika mabara matatu kwa lugha tatu tofauti ndani ya takriban miaka 1500 na waandishi zaidi ya 40 (waliotoka katika taaluma mbalimbali), biblia inabaki kitabu chenye kuhifadhi umoja kutoka mwanzo mpaka mwisho bila kujipinga chenyewe. Hali hii ni maalum kulinganisha na vitabu vyengine na inathibitisha kuweko kwa sauti ya Mungu ikinakiliwa na wanadamu.

Lengine katika ushahidi wa ndani, lapatikana katika unabii ulioorodheshwa ndani ya kurasa za biblia. Humu tunapata unabii juu ya mataifa binafsi kama vile Israeli, unabii wa miji Fulani, unabii wa maisha ya wanadamu na hata wa kuja kwake masihi, mwokozi si wa Israeli tu bali hata kwa wale pia watakaomwamini. kinyume cha unabii unaopatikana katika vitabu vyengine ama ule uliofanywa na Nostradamus, unabii wa kibiblia unatimia. Kuna unabii zaidi ya mia tatu kuhusu Yesu kristo katika Agano la kale pekee. Haikutabiriwa tu atazaliwa wapi na atakuwa wa jamii gani lakini pia ya kuwa angekufa na kufufuka siku ya tatu. Hakuna njia mwafaka ya kuelezea ni kwa uwezo gani unabii huu ulitimizwa ispokuwa kukiri ni kwa uwezo wa Mungu. Hakuna kitabu chenginecha dini chenye unabii unaodhihirika kama Biblia.

Ushahidi wa tatu unapatikana katika uweza na mamlaka ya Biblia. Hili si jambo dogo la kupuuzwa. Biblia ina mamlaka kuliko vitabu vyovyote vyengine. Uwezo huu unaonekana katika maisha ya wanadamu kama vile watu wasiohesabika wameweza kubadilishwa kwa kusoma biblia. Wenye kutumia mihadharati wameponywa na biblia, wahalifu sugu pia wamebadilishwa na biblia, wenye dhambi hukaripiwa na biblia na chuki kubadilishwa kuwa upendo kwa kulisoma biblia. Biblia ina uwezo wa kubadilisha maisha ya mtu kwa kuwa ni neno la Mungu.

Mbali na ushahidi wa ndani ya biblia, kuna ushahidi wa nje ya biblia unaothibitisha kuwa biblia kweli ni neno la Mungu. Umakini wa historia kama inavyoelezewa katika biblia ni ushahidi pia. Kupitia watafiti wa mabaki ya vitu vya kale na vitabu vyengine vilivyoandikwa, ratiba ya kihistoria katika biblia imehakikishwa mara kwa mara kuwa ya kweli. Watafiti hao pamoja na majarida wanayoyaandika husema ya kwamba biblia ndicho kitabu chenye kuongoza vyema katika historia sahihi ya maeneo mbalimbali. Jinsi biblia ilivyohifadhi histiria sahihi ya vizazi mbalimbali ni thibitisho ya kuwa ni kitabu cha ukweli pia katika kushughulikia maswala ya dini na mafundisho yake. Hili pia huthibitisha ya kuwa hili kweli ni neno la Mungu.

Jambo lengine ni kwamba heshima ya waandishi wa habari hizi za biblia. Mungu aliwatumia watu wa tabaka mbalimbali kuandika habari hizi. Tukuchunguza maisha ya watu hawa na ya kwamba walikuwa tayari hata kufa kwa ajili ya uaminifu wao kwa Mungu kwa ajili ya yale waiyoyaamini; Inathibitisha kuwa, watu hawa wanyonge na waaminifu walikuwa na uhakika kwamba Mungu kweli alikuwa amezungumza nao. Wale waliondika agano jipya na mamia ya waumini wengine (Wakorintho wa kwanza 15:6) walijua ukweli wa ujumbe wao kwa kuwa walikuwa wamemuona na kushirikiana na Yesu kristo baada ya kufa. Mabadiliko ya kumuona kristo aliyefufuka yalipokewa na uzito mkuu na watu hawa. Walibadilika kutoka kwa uoga wa kujificha na kuwa watu ambao hawaogopi kufa kwa ajili ya ujumbe wa Mungu uliokuwa umefunuliwa kwao. Maisha yao na vifo vyao vinathibitisha ya kwamba kweli biblia ni Neno la Mungu.

Ushahidi mwengine ni katika ile hali ya kutokuharibiwa kwa biblia. Kwa sababu ya umuhimu wake na kwamba ni neno la Mungu, biblia imepitia mapambano hatari mengi katika majaribio ya kuliharibu biblia kuliko kitabu chochote chengine katika historia Kutoka watawala wa jadi wa kirumi kama Diocletian, kupitia madikteta wa kikomiunisti na wale wasioamini kuna Mungu wanaoisho siku hizi, biblia imedhibiti hali yake na kudumu zaidi ya wapinzani wake. Hata sasa ndicho kitabu kinachochapishwa kwa wingi duniani.

Vizazi vyote na nyakati zote duniani,wapinzani wamekuwa wakipuuza biblia na kusema ni hadithi tu za watu lakini watafiti wa kihitoria wadumu wakithibitisha ya kuwa biblia ni kitabu cha kweli. Pia wapinzani wake wameshutumu mafundisho yake kuwa ya kijadi nayaliyopitwa na wakati lakini wema wake na mfumo wake wa kisheria umekubalika katika jamii na mila mbalimbali duniani kote. Inaendelea kushambuliwa na sayansi, saikologia, na vyama vya kisiasa na bado biblia inabaki na umuhimu sawa na ule iliyokuwa nao wakati ikiandikwa. Ni kitabu kilichobadilisha maisj\ha na tamaduni kwa muda wote wa miaka 2000 iliyopita. Haijalishi wapinzani wake wanapambana ki vipi, biblia inabaki ikiwa ni kitabu chenye nguvu, kweli na umuhimu sawa na ule kilichokuwa nao kabla kupigwa vita. Kuhifadhika kwa hali yake ya asili hata baada ya mashambulizi haya yote ni ishara ya kuwa biblia ni neno la Mungu. Isitushangaze ile hali ya kuwa bilia inapigwa vita na kuibuka bado mshindi bila madhara yoyote. Kumbuka Yesu alisema, “ Mbingu na dunia vitapita, lakini neno langu halitapita kamwe” (Marko 13:31). Baada ya kupitia ushahidi huu mtu bila shaka anaweza kusema “kweli Biblia ni Neno la Mungu.”

Tuwe makini, ndoa si jambo la mchezo!!


Katika maisha ya mwanadamu, kuna mambo mawili yaliyo muhimu zaidi. La kwanza ni uamuzi wa kumfuataYesu na la pili ni uamuzi wa kuoa. Tafakari, kuoa si sawa na kununua shati. Ukilichoka na shati unaweza kununua nyingine lakini, huwezi kumwacha mke wako hata kama ukimchoka. Neno la Mungu linatuonya hatari ya kuoa mwanamke asiye mchaji wa Mungu; Twasoma: “Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi” (Mithali. 21:19). “Kutonatona daima siku ya mvua nyingi, na mwanamke mgomvi ni sawasawa; 16atakaye kumzuia huyo huuzuia upepo” (Mithali. 27:15-16). Zingatia: Pengine mtu atasema, “mchumba wangu ana imani tofauti, walakini tukioana nitamfundisha.”Lakini ikumbukwe mara nyingi, baada ya kufunga ndoa, watu hubadilika asitake kufundishwa tena.Tukumbuke mfalme Sulemani alikuwa na hekima kuliko wanadamu wote. Walakini, alipata hasara kubwa kwa sababu aliwapenda wanawake wageni wasio mcha Mungu na matokeo yake badala ya kuwafundisha imani yake, “yeye mwenyewe alinaswa na imani yao” (1Wafalme 11:1-4). Basi tujiulize, je sisi tunayo hekima kuliko Sulemani? Ni bora mtu amfundishe mchumba kabla hawajaoana na kuhakikisha kuwa ameamua kumfuata Bwana kwa moyo wake wote na si kwa sababu ya ndoa, ndipo atakapokuwa na amani na furaha katika ndoa yake. Tukumbuke faida moja wapo ya kuoa katika katisa ni kupata mke alifundishwa maadili na wanawake waliomtangulia; Twasoma: “Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wautakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema; ili wawatie – wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na uwapenda watoto wao; na kuwa wenye kiasi, kuwa safi,kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe, ili neno la Mungu lisitukanwe” (Tit. 2:3-5). Hivyo ni dhahiri kuna faida kwa mkristo kujipatia mke aliyefunzwa maadili ya ndani ya kanisa. Zingatia: Kuna baadhi ya watu wamevutwa sana na maumbile au mambo ya kimwili ya wachumba wao lakini Biblia inatukumbusha kuchunguza mioyo yao zaidi kuliko sura ya nje; Tasoma: “Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa” (Mithali. 31:30). “Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana” (Mithali 19:14). Je unazijua sifa za mke mwema? Mungu ameeleza peupe; Soma: (Mithali 31:10-31)
HATARI YA KUOANA NA ASIYE MCHAJI WA MUNGU
Kama tulivyojifunza hako juu hatari moja wapo ya kuoana na wasio wachaji wa Mungu ni kuishia kuvutwa na upotofu na kuanguka kiimani; Twasoma:”Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye atakuangamiza upesi” (Kumbukumbu 7:4). Na hayo ndiyo yaliyomapata Suleima kama tulikwisha kuoona; Soma tena: (1 Wafalme 11:1-4) Tukumbuke ikiwa tutaanguka katika uovu, mwisho wake utakuwa ni kutupwa katika hukumu (adhabu ya milele); Twasoma: “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uachafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui,ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayo fanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Galatia 5:19-21) “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauwaji, na wazizi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili” (Ufunuo 21:8) “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani hilo ziwa la moto. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:14- 15) Zingatia: Ndoa ni kifungo hivyo tukumbuke tunapoana hatuna ruhusa ya kuacha hata kama wenzi wetu ni wabaya vipi; Twasoma: “Lakini wale waliokwisha kuoana nawagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; lakini ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.” (1 Wakorintho 7:10-11) “Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumwe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu.” (1 Wakorintho 7:39)
Hivyo ni dhahiri tunaaswa kuwa makini tunapo wachagua wenzi wetu, tukikumbuka ya kuwa kifungo cha
ndoa ni mpaka kifo

Wednesday, October 16, 2013

Yesu ni nani?


Yesu wa Nazareti ni nani kwako? Maisha yako hapa duniani na ya milele yanaguswa na jibu lako kwa swali hili?

dove
Nani, kwa maoni yako, ni...
  • Mtu wa ajabu kupita watu wote katika nyakati zote?
  • Nani aliyejitokeza kuwa mtu mashuhuri kwa vipindi vyote?
  • Kiongozi mkuu?
  • Mwalimu mkuu?
  • Mtu aliyefanya matendo mema kwa wanadamu kupita mwingine?
  • Mtu aliyeishi maisha matakatifu kuliko yeyote aliyewahi kuishi?
Tembea sehemu yoyote ulimwenguni. Ongea na watu wa dini yoyote. Haijalishi jinsi walivyoshikilia tabaka za dini zao, kama wanajua chochote kuhusu historia, watakubali kwamba hakujawahi kuwa na mtu kama Yesu wa Nazareti. Yeye ni mtu wa ajabu mno kuliko watu wote wa enzi zote.

Yesu alibadilisha mwenendo wa historia. Hata tarehe kwenye gazeti lako la leo inathibitisha kwamba Yesu wa Nazareti aliishi ulimwenguni karibu miaka 2,000 iliyopita. Maandishi kwa Kiingereza "B.C." yanasimamia nyakati kabla ya kuzaliwa kwa Kristo; vilevile maandishi "A.D." yanasimamia nyakati baada ya kuzaliwa kwa Kristo.
KUJA KWAKE KULITABIRIWA
Mamia ya miaka hata kabla ya Yesu kuzaliwa, maandiko yaonyesha wanabii wa Israeli wakitabiri kuja kwake. Agano la kale, lililoandikwa na watu wengi katika muda wa miaka 1,500, lina unabii zaidi ya 300 kuhusu kuja kwa Yesu. Yote yaliyotabiriwa yalitendeka, pamoja na kuzaliwa kwake kimiujiza, maisha yake matakatifu, kufa na kufufuka kwake.

Maisha aliyoishi Yesu, miujiza aliyotenda, maneno aliyosema, kufa kwake msalabani, kufufuka kwake, kupaa kwake mbinguni - yote yathibitisha kwamba yeye hakuwa mwanadamu peke yake bali alikuwa zaidi ya mwanadamu. Yesu alisema, "Mimi na Baba tu umoja" (Yohana 10:30), "Aliyeniona mimi amemwona Baba" (Yohana 14:9) na, "Mimi ndimi njia, na ukweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi." (Yohana 14:6).
MAISHA  NA UJUMBE WAKE HUSABABISHA MABADILIKO
Tazama maisha na mvuto wa Yesu wa Nazareti, Mesiya, katika historia yote na utaona kwamba yeye na ujumbe wake huleta mabadiliko makubwa katika mataifa na maisha ya wanaume na wanawake.5000 Popote mafunzo yake yalipoenea, utakatifu wa ndoa, haki na sauti ya wanawake imetiliwa maanani; shule na vyuo vikuu vimeanzishwa; sheria za kulinda watoto zimeandikwa; utumwa umeachishwa; na mabadiliko mengine mengi yamefanywa kwa manufaa ya wanadamu. Maisha ya watu binafsi yamebadilishwa kiajabu. Kwa mfano, Lew Wallace, jemedari aliyejulikana na mwandishi shupavu, alikana Mungu yupo. Kwa miaka miwili, Bw. Wallace alisoma kwenye maktaba zilizo bora sana kule Ulaya na Merikani, akitafuta habari ambazo zingeangamiza kabisa dini ya Kikristo. Alipokuwa akiandika sura ya pili ya kitabu hicho, alijikuta ghafla ameanguka magotini na kulia kwa Yesu akisema, "Bwana na Mungu wangu."
Kwa sababu ya ushuhuda usioweza kukanwa, hakuweza kuendelea kukana kwamba Yesu Kristo alikuwa mwana wa Mungu. Baadaye, Lew Wallace aliandika kitabu kilichoitwa "Ben Hur", moja wapo ya vitabu shwari vilivyo andikwa katika lugha ya Kiingereza kuhusu nyakati za Kristo.

Vile vile, marehemu C. S. Lewis, profesa wa chuo kikuu cha Oxford, alikana kwamba Kristo alikuwa pia Mungu kwa miaka mingi. Lakini, yeye pia, kwa hekima za ukarimu, alijinyenyekeza mbele za Yesu kama Mungu na Mwokozi baada ya kusoma ushahidi usio na pingamizi kwamba Yesu pia alikuwa Mungu .
BWANA, MWONGO AU MWENDA WAZIMU?
Katika kitabu chake kilichojulikana sana "Mere Christianity", Lewis aliandika, "Mtu ambaye alikuwa mwanadamu peke yake na kusema maneno kama aliyoyasema Yesu hawezi kamwe kuwa mwalimu wa utu wema. Huenda ikawa alikuwa mwenda wazimu - sawasawa na mtu anayesema kwamba yeye ni yai lililochemshwa - au roho chafu kutoka kuzimu. Wewe lazima uchague. Kama yeye alikuwa, na hata sasa ni Mwana wa Mungu, au yeye ni mwenda wazimu au kitu kibaya zaidi. Unaweza kumwita mpumbavu au unaweza kujinyenyekeza chini ya miguu yake na kumwita Bwana na Mungu. Lakini tusije na maneno hohehahe tukisema kwamba yeye alikuwa mwalimu shupavu wakibinadamu tu. Yeye hajaacha hilo chaguo wazi kwetu."

Yesu wa Nazareti ni nani kwako? Maisha yako ya hapa duniani na pia ya uzima wa milele yatategemea jibu lako kwa swali hili.

Dini zote zingine zilianzishwa na wanadamu na zinategemea falsafa za kibinadamu, kanuni na pendekezo za tabia. Ondoa waanzilishi wa dini hizi kutoka idhini na tabaka za kuabudu, na machache sana yatabadilika. Lakini ondoa Yesu Kristo kutoka Ukristo na hakuna chochote kitakachobaki. Ukristo uliopendekezwa kwenye Biblia siyo falsafa ya maisha peke yake, wala siyo tabaka na njia za kimila za kuabudu. Msingi wa Ukristo wa kweli ni uhusiano wa kibinafsi na Mwokozi na Bwana aliyefufuka na anayeishi.
MWANZILISHI ALIYEFUFUKA
Yesu wa Nazareti alisulubiwa, akazikwa kwenye kaburi lililokopwa, na siku ya tatu alifufuka kutoka wafu; Ukristo niwa kipekee kwa ajili ya jambo hili. Ubishi wowote juu ya ukweli wa Ukristo utategemea uthibitisho wa kufufuka kwa Yesu wa Nazareti.

Katika enzi zote, waliohitimu katika masomo na kuchunguza sana mathibitisho ya ufufuo wameamini, na wangali wanaamini kuwa Yesu yuhai. Baada ya kuchunguza mathibitisho ya ufufuo kama yalivyoandikwa na waandishi wa Injili, marehemu Simon Greeleaf, aliyehitimu kwa mambo ya kisheria katika Harvard Law School, alisema; "Haingewezekana kamwe kwao kuendelea kusisitiza ukweli wa mambo walionena, kama Yesu kweli hakufufuka kutoka wafu, na kama hawakujua jambo hili kama walivyojua ukweli wowote mwingine walioujua kwa uhakika.
John Singleton Copley ambaye ni mwanasheria aliyetambulikana sana, alisema: "Najua kiasi kwamba ushahidi ni kitu gani; nakwambia, ushahidi kama ule uliotolewa kuthibitisha ufufuo bado haujawahi kuvunjwa."
SABABU ZA KUAMINI
Ufufuo ni msingi katika imani ya Mkristo. Kuna sababu kadha wa kadha ambazo wale wanaosoma kuhusu ufufuo wanaamini kuwa ufufuo ulitendeka:�
boatKUTABIRIWA: Kwanza, Yesu alitabiri habari za kifo chake na ufufuo na zikatendeka kadri na jinsi alivyotabiri ( Luka 18:31-33).

KABURI LILIYO WAZI: La pili, ufufuo ni kielelezo cha pekee cha kaburi lililo wazi. Ukisoma Biblia kwa makini, utaona kwamba kaburi ambalo walilolaza mwili wa Yesu lililindwa barabara na wanajeshi wa Kirumi na pia lilizibwa na jiwe. Kama Yesu hakuwa amekufa, bali alikuwa amedhoofika - kama wengine walivyosema, walinzi na jiwe pia lingezuia juhudi za kuhepa au kusaidiwa na wafuasi wake. Maadui wa Yesu hawangechukua mwili kwa sababu kukosekana kwa mwili huo pale kaburini ingalitia nguvu imani juu ya kufufuka kwake.
KUONANA KIBINAFSI: La tatu, ufufuo ni kielelezo cha kipekee cha kuonekana kwa Yesu na wafuasi wake. Baada ya kufufuka kwake, Yesu alionekana mara zisizopungua 10 na wale waliomjua na pia kwa watu 500 waliokusanyika pamoja. Bwana aliwathibitishia kwamba kuonekana kwake mara tatu hizikuwa ndoto. Alikula na kuongea nao na walimgusa ( 1 Yohana 1 :1).

KUZALIWA KWA KANISA: La nne, ufufuo ni sababu ya pekee ya kueleza sababu ya kanisa kuanzwa. Kanisa la Kristo ni chama kikubwa kuliko vingine vilivyoko sasa pia vilivyowahi kuwepo katika historia ya ulimwengu. Zaidi ya nusu ya mahubiri ya kwanza yaliyohubiriwa yalikuwa kuhusu ufufuo (Matendo 2:14-36). Hakika kanisa la kwanza lilijua kwamba jambo hili litakuwa msingi wa ujumbe wake. Maadui wa Yesu wangelikomesha wakati wowote kwa kuutoa mwili wa Kristo.

MAISHA YALIYOBADILISHWA:
 La tano, ufufuo ni kielelezo cha kipekee cha maisha yaliyobadilishwa ya wafuasi wake. Walimwacha kabla ya kufufuka kwake; baada ya kifo chake walikufa moyo na kuogopa. Hawakutarajia kwamba Yesu atafufuka kutoka wafu (Luka 24 :1-11).

Lakini baada ya kufufuka kwake na mambo waliyopata wakati wa Pentekote, hawa waliokufa moyo, waliopoteza hamu, wanaume kwa wanawake, walibadilishwa na nguvu za Kristo aliyefufuka. Katika jina lake, walifanya kishindo kikubwa duniani. Wengi walipoteza maisha yao kwa ajili ya imani yao; wengine waliudhiwa vibaya. Matendo yao ya ujasiri hayana kielelezo kamili isipokuwa kwamba waliamini Yesu Kristo kweli alifufuka kutoka wafu - jambo lililowatosha hata kukubali kufa kwa ajili yake.

Katika miaka 40 ya kufanya kazi na wataalamu wa vyuo vikuu ulimwenguni, sijawahi kukutana na mmoja ambaye ameyasoma mathibitisho ya dhati kuonyesha uungu wa Yesu wa Nazareti na pia kufufuka kwake, ambaye hakukubali kwamba yeye ni Mwana wa Mungu, Mesiya aliyeahidiwa. Ijapokuwa wachache hawaamini, wanasema kwa moyo wa kweli, "Sijachukua muda wowote kusoma Biblia au kuangalia mambo katika kihistoria yalitotendeka katika maisha ya Kristo."
jesusandgirlBWANA ANAYEISHI:  Kwa sababu ya ufufuo wa Yesu, wanafuasi wake wa kweli hawafuati tu orodha za mwanzilishi aliyekufa, bali wanauhusiano wa karibu na wakibinafsi na bwana aliyehai. Yesu Kristo yuhai leo na anabariki na kuimarisha maisha ya wote wanaomwamini na kumtii. Katika enzi zote, wengi wamedhihirisha kufa kwake Yesu Kristo, kati yao wakiwa watu waliotenda makuu ulimwenguni.

Mwanafizikia na mwanafalsafa wa Kifaransa Blaise Pascal alisema jinsi mwanadamu anavyomhitaji Yesu aliposema, "Kuna pengo katika moyo wa kila mwanadamu linayoweza kuzibwa na Mungu peke yake kupitia Mwana wake Yesu Kristo."
Je, ungependa kumjua Yesu Kristo kama Mwokozi wako? Unaweza! Yesu anahamu ya kuanza uhusiano wa kibinafsi uliojaa upendo kwako. Ameshafanya matayarisho yote.
Kujua jinsi ya kuanza uhusiano na Kristo aliyehai, bonyeza hapa...

Tuesday, June 25, 2013


Awana (derived from the first letters of Approved Workmen Are Not Ashamed as taken from 2 Timothy 2:15) is an internationalevangelical nonprofit organization founded in 1950, headquartered in Streamwood, Illinois. The mission of Awana is to help "churches and parents worldwide raise children and youth to know, love and serve Christ."[1] Awana is a non-denominationalprogram and licenses its curricula to any church willing to pay for and use the Awana materials consistent with its principles. In addition to its programs for children and teenagers, Awana has prison ministries, and a parallel curriculum for family use – the "Awana-At-Home" series.

Contents

  [hide

Curricula[edit]

Awana offers multiple curricula levels from toddlers to senior high-school. In the U.S. and Canada, Awana is split into six age groups: Puggles (2 yr olds), Cubbies (3 & 4 yr old or "the 2 years prior to Kindergarten"), Sparks (Kindergarten, Grade 1 & 2), Truth & Training (T&T) (for grades 3, 4, 5 & 6), Trek (grades 7, 8, 9) and Journey (High school). Most recently T&T divided up into Pals (Boys Grade 3 & 4), Chums (Girls Grade 3 & 4), Pioneers (Boys Grade 5 & 6), and Guards (Girls Grade 5 & 6), which changed in the late 1990s. Originally Pals and Chums were Grades 3 to 5 and Pioneers and Guards included Grades 6 to 8. Trek and Journey, which are under the 24/7 Ministries banner, were called, respectively, Jr. Varsity and Varsity. Internationally, the age groups offered vary in each country and materials are available in many languages. Awana's prison ministries (Malachi Dads) attend the needs of inmates by providing parental coaching to incarcerated fathers, and to children of inmates by sponsoring events in prisons to bring children and their inmate fathers closer together.
Puggles has three "friends" in the materials  – Sydney the Koala, Alice the Kangaroo, Puggle the Platypus. The precepts taught are that "God made all things", "give thanks" and "God is love".
Cubbies friends include Cubbie Bear, Ern E. Elephant and Luv E. Lamb. This material is currently being updated and new materials are to be implemented fall 2013. Current handbooks are "Hopper" and "Jumper".
Sparks friends include Sparkie the firefly and children named Chloe, Joel, Jacob and Chloe's dog Sebastian. The original three-book series was called Skipper, Hiker and Climber but this material was updated 2009-2011 and are now called HangGlider, WingRunner and SkyStormer. If a clubber completes all three books they earn the Sparky Award Plaque.
T&T (truth and training) friends include children and the dog, Streamwood. The books are called Ultimate Adventure 1 and 2 and Ultimate Challenge 1 and 2. There is an award for each book completed between Grade 3 to Grade 12  – Alpha Award (one book), Excellence Award (two books), Challenge Award (three books) and Timothy Award (four books).
Trek is based on a travel theme. It has three years worth of lessons so the program can be used for Grades 6, 7 and 8 depending on local school and church preferences. The three years are called the Billboard, Roadsign and Dashboard Series. Additional awards available are the Milestone Award and Meritorious Award (six books between Grade 3 to Grade 12).
Journey is based on Bible studies of individual books of the Bible with some optional topical studies (12 weeks each). Each year there is one study that is chosen by Awana for all clubs to use if they plan to participate in quizzing. To complete a year of Journey curriculum, students must complete the Faith Foundation (a small booklet containing a few verses), two studies and read one-quarter of the Bible (books are specified). If a student completes all 10 years of material from Grade 3-12, the Citation Award is awarded. This is the highest level of achievement and considered a great honor.

Awana events[edit]

Awana missionaries and volunteers run local, state (provincial) and regional competitions between churches' Awana programs. These involve Bible Quizzing, AwanaGames, Sparks-A-Rama, and Awana Grand Prix. High-school age Awana students can also participate in an annual national event called Summit.
Awana missionaries help churches start the Awana ministry, train church leaders how to introduce kids and youth into the Awana program and instruct church leaders at Awana Ministry Conferences on how to better utilize the Awana ministry.
Awana missionaries are completely "faith supported" by donations from churches and individuals, thereby acquiring all of the funds necessary to keep each of their ministries funded in addition to receiving all funds needed for their personal housing and income needs.

Non-profit status[edit]

Awana broadly encompasses the following tax-exempt entities:
  • Awana International;
  • Awana Clubs International;
  • Awana International Canada
  • Impact Life, and;
  • Canadian Adventure, Inc.
According to the 2006 Form 990 filed with the IRS by Awana Clubs International, ACI reported gross revenues of $45,595,800 --- significantly higher than the amounts reported for both 2004 ($41,464,006) and 2005 ($41,513,499) within the Awana "2004–2005 Financial Highlights" report,[2] but this gross revenue variation may be due to a timing difference with the actual start and end date of the ACI tax year or a transfer of funds between the various Awana EOs.[3]
At the close of 2007, Awana was named one of 30 "Shining Light Ministries" by MinistryWatch.com, a financial watchdog group. The award is based on passing a number of stringent financial accounting and reporting standards.[4] Awana is also a member of the Evangelical Council for Financial Accountability (ECFA).

See also[edit]

References[edit]

External links[edit]


Thursday, November 22, 2012

JE! MUNGU NA YESU NI MMOJA?


Makanisa ya Kikristo yanafunza ya kuwa Yesu Kristo si kama kuwa ni Mwana wa Mungu tu, bali hakika ni Mungu khasa.  Baba, Mwana na Roho Mtakatifu ni mmoja.  Watatu katika mmoja, na mmoja katika watatu.  Wote ni wa milele, wote ni sawa.  Yesu ni Mungu, na Mungu ni Yesu. Hiyo ni imani ya Kikristo, ambayo inaaminiwa na karibu Wakristo wote.  Hebu tuifunue Biblia tutazame inasema nini katika jambo hili?
Mt Paulo katika barua yake ya kwanza kuwapelekea Wakorintho aliandika:
Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.
1 Wakorintho 15.15
Juu ya kuwa Paulo anaambiwa ya kuwa akiamini kuwa Masihi (yaani Kristo) na Mwenyezi Mungu ni kitu kimoja hapa anasema: "Tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo." Ikiwa Mungu kamfufua Kristo, hawawezi kuwa wote wawili hao ni mtu  mmoja. Mmoja alikuwa ni mtenda, mfufuaji, na wa pili alikuwa ni mtendwa, mfufuliwa. Kama Kristo ni Mungu mwenye uwezo wa kufufua basi maelekeo ni kusema: "Kristo kajifufua", sio kafufuliwa. Mwenye kufufuliwa ni mfu asiyejiweza kitu.
Katika kitabu cha Matendo ya Mitume inasimuliwa kuwa Mt Stefano alisema aliyoyaona yaliyo mbinguni. Alisema:
Tazama!  naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
      Matendo 7.56
Mwana wa Adamu ndiye Yesu, na kwa jina hilo ndio mwenyewe akipenda kujiita, sio Mwana wa Mungu. Hapo basi huko mbinguni Stefano anasema anamwona Yesu kakaa mkono wa kulia wa Mungu. Mwenye kukaa mkono wa kulia wa fulani hawezi kuwa ndiye yule yule fulani. Hayo ni maelezo ya mbinguni.  Ni wazi basi kwa ushahidi wa Biblia kuwa Yesu hakuwa Mungu mbinguni kama alivyokuwa si Mungu duniani.
Yesu alipokimbilia kwenye Mlima wa Zaituni na huku akisakwa na Mayahudi alijitenga na wanafunzi wake.  Huko faraghani aliomba hivi:
Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.  Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.
  Luka 22.42-43
Hapa tunaona mambo matatu muhimu:
  1. Yesu anamwomba Mungu. Yesu anamwabudu Mungu. Wawili hao ni mbali mbali, na vyeo vyao ni mbali mbali. Yesu ni mtumwa mnyonge mwenye kuomba na kuabudu. Na Mungu ni Mwenyezi Mungu mwenye uwezo wote na mwenye kustahiki kuabudiwa pekee, hata na Yesu, mwenye kutakiwa msaada pekee, hata na Yesu.
  2. Mapenzi ya Mungu ni mbali na yale ya Yesu. Yesu hataki kuuliwa, ananyenyekea na kuomba kwa Bwana wake: "uniondolee kikombe hiki" cha mauti.  Yesu hana azma hata chembe ya kufa msalabani, kifo cha mhalifu, kifo cha laana kama maadui zake  Mayahudi walivyoazimia kumpatilisha nacho. Lakini anakiri kuwa ni mapenzi ya Mungu sio yake yeye yatendeke. Yeye hana hila wala nguvu za kuzuia kudra ya Mwenyezi Mungu.
  3. Yesu, Mwana wa Adamu, anakata tamaa. Imani inampunguka. Kavunjika moyo. Ikabidi "Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu."
Jee, yaelekea kuwa Yesu ndiye Mungu? Yaelekea kuwa yeye na Mungu kuwa ni sawa? Kama upo wasiwasi wo wote wa kujibu hayo, mwenyewe Yesu anajibu kama anavyo hadithiwa na Yohana kuwa kasema:
Baba ni mkuu kuliko mimi.
Yohana 14.28
Na mwishoni naye yupo mslabani:
Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani?  yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?
Mathayo 27.46
Yafaa hapa tujiulize: Yesu akimlilia Mungu gani hapo msalabani ikiwa naye mwenyewe ni Mungu? Au nini alikusudia aliposema: "Mungu wangu naye ni Mungu wenu"?  Maneno hayo kama yanaonyesha cho chote basi yanaonyesha unyenyekevu wa Yesu mbele ya Mungu wake.  La kustaajabisha ni kule kukata tamaa kwake na kuvunjika moyo.  Huwaje mtu wa imani, licha ya nabii na mwana pekee wa Mungu, akate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu.  Ama kuwa Mungu akate tamaa na Mungu, na kumyayatikia: "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha", ni jambo ambalo halimkiniki kuwa.
Kwa uthibitisho ulio wazi Biblia inatwambia kuwa Yesu si Mungu, wala Mungu si Yesu. 

Tuesday, November 13, 2012

FAHAMU NINI MAANA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA BIBLIA

 Mt. Meshack Ezekia Kitova    phone;0757672626

 Nini maana ya kusifu na kuabudu


KUSIFU NA KUABUDU ni maneno tofauti na yana maana tofauti
1. kusifu

MAANA --- nikuelezea wasifu au wajihi za kitu au mtu. Sasa tunaposema tunamsifu Mungu inamaanisha ni KWA KUMUINUA JUU, KUSHUKURU KUMPAZIA SAUTI,KUFANYIA SWANGWE, KUJISHUSHA CHINI YAKE KWA UNYEYEKEVU,nk Zaburi 100:4

Neno hili kusifu kwa kiebrania lilikuwa na maana ya;
Tehila, yaani kutamka neno kwa kuongeza vionjo na mbwembwe zaidi. Mfano neno haleluya unalitamka (Ha, ha leluya huuu eee) Tehila ni kuwa kama kichaa unaposifu au kuabudu kwa utukufu wa Bwana. (Nilidhani labda hapa ndipo waswahili walipopata neno taahila).

Yadaa yaani kujiachia kwa Mungu (you just surrender yourself to the Lord).
Barak yaani kusaluti mbele za Bwana. Ni kuonyesha kwamba ni yeye peke yake anayestahili heshima na utukufu. Huwezi kumpigia saluti mtu usiyemwona, hivyo ni kwa njia ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli ndipo tunapomwona kama alivyo na utukufu wake

2. Kuabudu
Neno la Kiebrania shachah lina maana ya kuabudu, kusujudia, kuinama kwa kuonesha unyenyekevu, kuonesha heshima kubwa au kuanguka kifudifudi. Neno la Agano la Kale proskuneo halikadhalika lina maana ya kubusu mkono, au kupiga magoti na kugusa ardhi kwa paji la uso kwa unyenyekevu mkuu. Maneno mengine mawili ya kuabudu yana maana ya kutumika, kufanya ibada Takatifu na kumtolea Mungu Sadaka.

Waache Watu Wangu Waondoke, Ili Wapate Kunitumikia, Dai hili Mungu alilolirudia mara kwa mara lilipelekea Farao kuwaruhusu watu wa Mungu kutoka Misri. Tangu wakati huo, Mungu, Mungu mwenye wivu, amekuwa akipambana na watu wake akiwazuilia kuabudu miungu mingine na sanamu, na badala yake wamwabudu Mungu aliye hai na wa kweli. Kutoka 7:16
Ibada ni kumtukuza Mungu na kumfurahia daima. Mungu anawatafuta watu wa kumwabudu, na kufanya ibada ndiyo wito wetu wa kwanza (Yn4:23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta. Msitari wa 24 unasema Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.). Ibada ya kweli ni pale tunapomruhusu Roho Mtakatifu atuongoze kutoka katika roho zetu au mioyo yetu kuabudu katika roho na katika kweli na sio tumaini letu ktk miiliau akili zetu Flp 3:3.

Ibada ni tendo la thamani kubwa, ni la kipekee na linamhusu Mungu (utatu mtakatifu) ambao peke yao wanastahili. Lucifer, aliyekuwa mhusika mkuu wa ibada huko mbinguni, alitaka ibada hiyo iwe kwa ajili yake, maana yake aabudiwe yeye badala ya Mungu; na hilo ndilo lililopelekea kuanguka kwake (Isaya 14 na Ezekieli 28). Hata wakati fulani alitaka Yesu amsujudie ili eti ampe falme zote za dunia lakini Bwana alikataa Mt4:8-10.

Kwa hiyo kuabudu ni ibada na tunaposema ibada sio zile taratibu za kibinadamu tulizojipangia katika ibada zetu za siku za leo, ibada za leo tumeweka mambo mengi sana na yanatumia muda mwingi sana kuliko ile maana hasa ambayo mungu aliikusudia katika agano la kale utana ibada zilikuwa zinafaywa kwa mambo makuu 2 neno la Mungu, na Kuabudu.

Kuabudu ni sehemu ya maisha wanadamu tumeumbiwa kuabudu, watuwezi kuishi bila kuabudu hapa haijalishi unaabudu nini!!! Unaweza kuwa unaabudu Mungu wa kweli au miungu kama ambavyo ukisoma bilia utaona kuna miungu mingi inatajwa mfano Baali, Dagon ink na hata leo iko miungu mingi ambayo wanadamu wanaiabudu lakini wa kuabudiwa ni mmoja tu. Na katika biblia tunaona kuaudu kwa mara ya kwanza kulikofanywa na Ibrahimu kutoka katika kitabu cha mwanzo 12: 8 Psalms 34:1 inaonyesha tunatakiwa kumwabudu Mungu kila wakati.

Kwanini tuabudu
kuabudu ni agizo kutoka kwa Mungu kutoka 20 2-4 . Psalm 96:9, Psalm 29:2 Tunapomwabudu mungu naye Mungu hufurahiwa na sisi Zephaniah 3:17 Rom 12:1-2

Your Worship = Your View of God
jinsi unavyoabudu ndiyo mwonekano wa mungu ulivyo ndani yako, haijarishi unaabudu wapi uwe peke yako au mko wengi kama unaabudu kwa kutokumaanisha au kumaanisha itajulikana tu na hivyo ndivyo mtu anaweza kujua ni jinsi gani mtazamo wako kwa Mungu wako.

KUNA NGUVU KATIKA KUSIFU NA KUABUDU
Yoshua 6:20 Matendo 16:23-26 zinaonyesha ambavyo kwa kutumia kusifu tu Mungu alishuka na kufanya lile lililokuwa hitaji lao.

Kusifu kunamfukuza adui
Psalms 50:23. 2 Nyak 20:22. Ukiwa unasifu na kuabudu humfukuza adui mbali kutokana na ukiwa kwenye ibada Mungu hushuka maana yeye anasema anakaa katikati ya sifa hivyo palipo na Mungu shetani hawezi kuwepo lazima akae mbali.akimbie mbali kabisa maana kunakuwepo na uwepo wa bwana wa Majeshi.

Je, ni wakati gani tuabudu?
Ni niyakati zote zinafaa kumwabudu Mungu. Kwa nyakati zilizotengwa Zaburi ya 100 inatuelekeza namna ya kuanza, lakini zaidi ya yote tunapaswa kuishi maisha ya ibada bila kukoma. Kwa kila tunapopumua, kwa kila wazo, kwa neno na tendo, tunapaswa kumwabudu Mungu wetu mzuri tunayemtumikia milele na milele Zab 145:1,2

mwa 12:6- Siku zilipita na watu wakafanyia ibada kwenye Hekalu na kwenye masinagogi; lakini siku hizi miili yetu ni hekalu la Mungu 1Kor 6:19 tu hekalu la Mungu sisi ibada zinatakiwa zifanyike kila wakati na si mara moja kwa wiki kama wengine wanavyo dhani.

Je, Tunafanyaje Ibada?
Biblia inatufahamisha jinsi watu walivyotumia mioyo yao, mawazo yao, mikono yao, viganja vyao, miguu yao, na midomo yao katika uimbaji. Walipaza sauti zao kwa furaha na kusujudu, kucheza, kusifu, kubariki na kushukuru.

Maneno kama halal na haleluya kutoka katika Zaburi yana maana ya kusifu, kumwinua na kumwadhimisha Bwana. Neno Yadah lina maana ya kunyoosha mikono hewani, na neno barak lina maana ya kupiga magoti katika ibada ya kumbariki Mungu. Kuitoa miili yetu katika kumhudumia Mungu na mwanadamu ni ibada pia (Rum 12:1). Watu pia humwabudu Mungu katika sanaa zao, katika uandishi wao, katika michezo ya kuigiza, katika muziki, katika usanifu wa majengo, na hata katika utoaji wa fedha zao kwa ajili ya Injili.

Kusifu na kuabudu sio kuimba tu
Watu wengi wanajua kuwa kusifu na kuabudu ni kuimba tu hapana kuna njia nyingi za kusifu au kuabudu, unaweza kutumia sanaa nyingine kumwabudu mungu au watu wengine wakamwabudu Mungu mf maigizo, ngonjera, shaili, uchoraji, upambaji au unakshi wa vitu, kujenga .nk

Ibada Kanisani
KatIka kanisa makusanyiko yetu yanapaswa kujawa na zaburi, nyimbo, na tenzi za rohoni ambazo zinaweza kuongozwa na Roho katika lugha mpya anazotupatia Yeye. Kwahiyo mikutano mingi ya kisasa haina tofauti sana na burudani za kikristo kama kwenye kumbi za starehe. Watu huwa wanaangalia tu, lakini je, wanaabudu? Uwepo wa Mungu na Roho wake katika ibada zetu utawafanya watu wasioamini kuanguka chini na kuabudu (Kol 3:16) (1Kor 14:15,16,25,26) (Efe 5:19) (Mdo 2:4).

Ibada Ya Kweli Ina Gharama
Biblia inazungumzia habari za sadaka za kusifu. Daudi alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote, na akakataa kumtolea Mungu kafara ambayo isingemgharimu cho chote (2Sam 6:14; 24:24). Wale mamajusi wa Mashariki walitoa zawadi za gharama kubwa walipokuja kumwabudu Yesu (Mt 2:9-12), na mwanamke mmoja alimpaka Yesu kwa mafuta ya gharama kubwa, akamwosha miguu yake kwa machozi yake, na kuifuta kwa nywele zake (Lk 7:36-50). Hivyo ibada yoyote inaambatana na kutoa tena vitu vyetu vya thamani.

Tunapaswa kumsifu Mungu kwa jinsi alivyo na kwa matendo yake; lakini Mungu mwenyewe anawatafuta na anawataka wafanya ibada, na si mradi ibada tu. Kusifu kwaweza kufanywa hadharani, lakini ibada mara zote ni jambo la ndani ya moyo. Kusifu mara zote kunaweza kuonekana au kusikika, lakini kuabudu yaweza kuwa ya kimyakimya na iliyofichika. Kusifu kunaonekana, kuna kutumia nguvu, kuna misisimko na furaha; lakini ibada mara zote ni heshima na hofu katika uwepo wa Mungu.
Biblia pekee inatuonesha jinsi Mungu anavyo hitaji na kutamani kuabudiwa na yeye pekee yake ndiyo anayestahili kuabudiwa.

Kusifu na kuabudu kwa siku za leo
Katika siku za leo kuna ufinyu wa mafundisho katika kusifu na kuabudu na ndiyo maana ya kuanda somo hili ili tupanuane mawazo. Watu wengi wa leo wanadhani kusifu ni kuimba kwa nyimbo zenye midundo ya harakaharaka(zouk&sebene) na ukipunguza spidi ndo kuabudu. Hasha tunaposema kusifu inatokana na maneno yaliyopon kwenye wimbo husika kweli ni ya kusifu, kama ni maneno ya kusifu tunasema ni wimbo wa sifa haijarishi speed inayotumika na hali kadhalika nyimbo za kuabudu. Watu katika kipengele hiki huwa wanachakanya nyimbo utakuta wakati wa kusifu anaimba wimbo wa kutia moyo au wa maombi, kinachotakiwa ni kujua kuwa kila jambo lina wakati wake ziiko nyimbo za mazishi, kufariji, kutia moyo, za maombi, za kusifu , na za kuabudu nk sasa usichanganye kwenye kusifu wewe unaimba parapanda italia au tuonane paradiso, hizo sio za sifa sasa najua wewe utafanya zoezi la nyimbo unazozijua ili kufahamu zina ujumbe gani na ziko katika kundi lipi kati ya hayo niliyokufundisha hapo juu.

Baadhi ya maandiko yanayo onyesha aina za kusifu na kuabudu kwa:

1. Kusimama (Zab 135:1-2, 134:1)

2. Kuinua mikono (Zab 134:2, 28:2)

3. Kuinama au kupiga magoti (Zab 95:6)

4. Kupiga makofi (Zab 7:1)

5. Kucheza (Zab 149:3, 150:4, 2Sam 6:14)

6. Kicheko (Zab 126:2, Ayu 8:20-21)

7. Kufurahi (Kumb 12:11-12, Law 23:40)

8. Kutembea (2Nya 20:21-22)

9. Shangwe (Zab 95:1)

10. Kupiga kelele (Zab 66:1, Law 9:23-24)

11. Kupiga vigelegele (Zab 33:1, 32:11)

12. Ukimya (Mhu 3:7)

13. Kupaza sauti (Isaya 12: 6, Zab 42:4)

14. Kulia/ kutoa machozi katika roho mtakatifu

Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa